Latest News


More

Posted on : Saturday, September 5, 2015 [0] comments Label:

SEMINA YA MWALIMU MWAKASEGE KUFANYIKA VIWANJA VYA CHUO KIKUU JIJINI DAR ES SALAAM

by : Unknown
Semina ya Neno la Mungu Mjini Dar es salaam.

  Kuanzia tarehe 06 hadi 13 Septemba, 2015 tutakuwa na semina Dar es salaam uwanja wa Chuo Kikuu (UD) ,kila siku kuanzia saa 9 alasiri hadi 12 na mbili jioni. 

    Usikose kushiriki kusikiliza neno la Mungu na Mwl. Christopher Mwakasege, wagonjwa na wenye shida mbalimbali pia wataombewa. Utaweza kutazama live kwa kupitia Ustream pia
by : Unknown

Kim Davies aliyekataa kusaini cheti cha ndoa Kentucky

Jaji mmoja nchini Marekani, ameagiza afisa mmoja wa serikali katika jimbo la Kentucky, kufungwa jela, baada ya kukataa kutekeleza agizo la mahakama la kutoa cheti rasmi cha ndoa, kwa wapenzi wawili wa jinsia moja.
Kim Davies amesema imani yake kama Mkristo, haimruhusu kusaini cheti kama hicho. Ndoa ya jinsia moja ilihalalishwa nchini Marekani Juni mwaka huu.
Umauzi huo wa Davis, wa kutosaini cheti hicho umepokelewa kwa hisia tofauti.
Kuna baadhi ya wale wanaomuona kama shujaa huku wengine wakisema ni msaliti.

Tofauti za imani

Davis ambaye ni karani wa mahakama, alikataa kutoa cheti hicho, kwa wanandoa hao katika kaunti ya Rowan iliyoko Kentucky.
Afisa huyo ambaye alichaguliwa na raia amesama, kitendo hicho kinakiuka maadili ya kidini.
Davis sasa ametupwa jela na jaji huyo kwa kudharau mahakama.
Amesema alikuwa amekula kiapo cha kuwa offisini na viapo vina maana nyingi.
Watu wanaoshabikia ndoa ya jinsia moja, walikusanyika nje ya mahakama, wakiimba kuwa mapenzi imeshinda na kusema kuwa sasa wanafuraha kwa sababu wanaweza kufunga ndoa.
Lakini kwa upande wake Kim Davis amepata uungwaji mkono kutoka kwa Wakristo wahafidina na baadhi ya wagombea wa urais wa chama cha Republican, ambao wanasema kuwa Davis amehukumiwa jela kwa kufuata imani zake.
by : Unknown

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mheshimiwa Paul Makonda jumapili hii alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa vitabu vya injili vya mwalimu Lilian Ndegi katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe

Bwana Makonda (pichani juu) alimshukuru mwalimu Lilian Ndegi jinsi Mungu anavyomtumia kuponya roho za watu kwa njia ya vitabu na alisema yuko tayari kushirikiana naye kuhakikisha vitabu hivyo vinawafikia watu wengi zaidi
 Pichani juu Bwana Makonda akikata utepe kuashiria uzinduzi wav itabu hivyo



Wakina mama wa kanisa waliandaa  keki maalum  kwa ajili ya mwalimu Lilian Ndegi

Bwana Makonda akimshukuru Tumaini Kichila kwa ununuzi wavitabu vya mwalimu Lilian Ndegi

 Mgeni rasm bwana Paul Makonda kushoto  akiwa na mtume Apostle Ndegi (mkuu wa kanisa la Living Water Center - Kawe) na mwalimu Lilian Ndegi ambaye ndiye mwandishi wa vitabu hivyo
 Wakina mama wa Kawe wakiunga mkono katika uzinduzi huo wa jumapili


 Badhi ya vitabu mbalimbali  (pichani juu na chini) ambavyo vimetungwa na mwalimu Lilian Ndegi




Wamama wa Kanisa la Living Water Center Waliandaa keki maalum kwa Mwalimu Lilian Ndegi
Mwalimu Lilian Ndegi akimlisha mumewe Apostle Ndegi Keki
Mwalimu Lilian Ndegi akimlisha mgeni rasmi bwana Paul Makonda keki



by : Unknown
Jumapili hii ilifanyoka ibada nzuri katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe ambapo kiongozi wa kanisa hilo Mtume Onesmo Ndegi  (pichani juu) aliongoza na kuhubiri
Pichani juu Mtume Onesmo Ndegi akimtambulisha ndugu wa mke wake Lilian Ndegi ambapo pamoja na mambo mengine kulikua na uzinduzi wa Vitabu vya mwalimu Lilian Ndegi (ambaye ni mke wa Mtume ndegi)
 Waumini wakifuatilia ibada hiyo jumapili katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe







Posted on : Friday, August 21, 2015 [0] comments Label:

SEMINA YA MTUMISHI WA MUNGU SETH OSCAR - MBEZI MWISHO (MAKABE) KANISA LA EAGT

by : Unknown
"KUTOKA KWENYE VIFUNGO"........ISATA 42:22
Mtumishi wa Mungu Seth Oscar anaendesha mkutano wa  injili katika kanisa la EAGT Mbezi Makabe
Mkutano huo umeanza jumatatu wiki hii na unaenda kuhitimishwa jumapili hii 
Pichani juu mtumishi huyo akihubiri katika mkutano huo wa injili


Pichani juu mtumishi wa Mungu akifungua watu kutoka kwenye vifungo mbalimbali vya ibilisi

 Watu mbalimbali wakifunguliwa kwenye mkutano huo wa injili

 Uponyaji ukiendelea kwenye mkutano huo






Posted on : Monday, August 17, 2015 [0] comments Label:

ASKOFU SHOO NDIYE MKUU WA KANISA LA K.K.K.T

by : Unknown
Askofu Mkuu mpya wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Frederick O. Shoo (kulia) akiwa na Askofu anayemaliza muda wake, Dk Alex Malasusa baada kuchaguliwa juzi usiku kwenye mkutano ulifanyika Arusha. Picha ya Mtandao 

Dar es Salaam. Askofu Dk Fredrick Shoo amechaguliwa kuwa Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), akichukua nafasi ya Dk Alex Malasusa aliyemaliza kipindi chake cha miaka minane.
Dk Shoo, ambaye pia ni askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, alichaguliwa juzi usiku katika siku ya tatu na ya mwisho ya mkutano mkuu wa 19 wa kanisa hilo uliofanyika Chuo Kikuu cha Tumaini (Tuma) jijini Arusha baada ya kuwashinda maaskofu wenzake wawili, katika uchaguzi uliokuwa na kila aina ya ushindani.
Waliokuwa wakichuana kuwania nafasi hiyo baada ya kupendekezwa na Halmashauri Kuu ya KKKT ni Askofu Dk Stephen Munga wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Askofu Charles Mjema wa Dayosisi ya Pare na Dk Shoo.
Mwenyekiti wa uchaguzi huo, Dk Malasusa, ambaye pia ni askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, alimtangaza Dk Shoo kuwa mkuu wa kanisa hilo kwa kipindi cha miaka minne baada ya kupata kura 153, huku Dk Munga akipata kura 67, ikiwa ni baada ya uchaguzi huo kurudiwa mara tatu kutokana na mshindi kutopata zaidi ya theluthi mbili ya kura zote.
Kanuni za uchaguzi za KKKT zinaeleza kuwa mshindi atapatikana kwa kupata kura zisizopungua theluthi mbili ya kura zote zilizopigwa, iwapo mshindi hatapatikana katika duru la kwanza, majina mawili yaliyopata kura nyingi ndiyo yatakayopigiwa tena kura.
Iwapo theluthi mbili haitapatikana katika duru la pili, kura ya wingi au uchache itatumika kwa duru la tatu ili kumpata mshindi.
Katika kuhakikisha mshindi anapatikana, mkutano huo ulilazimika kutumia hatua ya wingi wa kura na Dk Shoo kuibuka mshindi.
Katika awamu ya kwanza, Askofu Mjema alipata kura 53, Dk Munga kura 81 na Dk Shoo kura 86, idadi ambayo haikufika theluthi mbili ya kura zote kulingana na kanuni za kanisa hilo jambo lililosababisha uchaguzi kurudiwa mara ya pili.
Dk Malasusa alitangaza matokeo ya awamu ya pili ya kura zilizopigwa ambapo Askofu Munga alipata kura 94 na Dk Shoo kura 124. Kura moja ikiharibika.
Kabla ya kuanza kwa mkutano huo wajumbe wa Halmashauri Kuu walipitisha majina matatu ya maaskofu waliowania nafasi hiyo na kuyapeleka kwenye mkutano huo ili yapigiwe kura.
Wajumbe wa mkutano huo mara baada ya kupewa karatasi za kupigia kura walikwenda katika vyumba maalum kwa ajili ya kumchagua askofu wanayemtaka, mara baada ya kuchagua walitakiwa kurejea ukumbini na kutumbukiza karatasi hizo katika vifaa vilivyoandaliwa kuhifadhia kura hizo.
Kauli ya Dk Shoo
Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Dk Shoo alimshukuru Mungu huku akionyesha mshangao wa kuchaguliwa kwake.
“Sijui nimepataje nafasi hii, ni nguvu ya Mungu tu kwa kweli. Kwa ushirikiano wa waumumini wote nitaweza kufanya kazi hii, naomba mniombee,” alisema.
Alichokisema Malasusa
Akizungumza katika ibada ya kufunga mkutano huo uliomalizika saa 6:00 usiku, Dk Malasusa alisema anamuachia madaraka Dk Shoo katika hali ya amani na utulivu, huku akiwapongeza viongozi na maaskofu wote wa kanisa hilo.
Awali kabla ya kuanza kwa uchaguzi huo, mkutano huo ulimchagua Alice Mtui wa Dayosisi ya Konde kuwa mwandishi wa kanisa hilo kwa kipindi cha miaka minne.
Alice alipigiwa kura 201 na wajumbe wa mkutano huo, huku kura za hapana zikiwa 17 na kura moja ikiharibika.
(Chanzo: Mwananchi Communications)


Posted on : Tuesday, July 21, 2015 [0] comments Label:

UNAWEZAJE KUSHUGHULIKA NA WAKWE ZAKO?

by : Unknown

Kushughulika na Wakwe

KIKWAZO

“Mke wangu aliwaambia wazazi wake tulipokuwa tukikabili matatizo. Kisha baba yake akanipigia simu ili kunishauri jinsi ya kushughulikia hali hiyo. Sikufurahia jambo hilo!”—James. *
“Mara nyingi mama mkwe husema, ‘Ninamkosa sana mwana wangu!’ Husema pia jinsi walivyokuwa karibu na mwana wake, jambo linalonifanya nihisi hatia kwamba nilifunga naye ndoa na kumletea mama yake maumivu ya moyo!”—Natasha.
Je, inawezekana kuzuia hali ya kushughulika na wakwe isiwe tatizo katika ndoa?

UNACHOPASWA KUJUA

Ndoa huanzisha familia mpya. Biblia inasema kwamba mwanamume anayefunga ndoa “atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake.” Mke pia anafanya hivyo kuelekea wazazi wake na mume wake. Anapofunga ndoa, Biblia inasema kwamba wawili hao wanakuwa “mwili mmoja.” Wanaanzisha familia mpya.—Mathayo 19:5.
Ndoa yako inachukua nafasi ya kwanza badala ya wazazi wako.Mshauri wa ndoa, John M. Gottman aliandika hivi: “Jukumu moja la msingi katika ndoa ni kwa mume na mke kuwa na umoja. Kuanzisha au kuchochea hisi hiyo ya kufanya mambo kwa umoja na mwenzi wako huenda kukatia ndani kutoshughulika sana na watu wa familia zenu.” *
Huenda ikawa vigumu kwa baadhi ya wazazi kuzoea badiliko hilo.Mume mmoja kijana anasema hivi: “Mara nyingi mke wangu alitanguliza kutimiza mahitaji ya wazazi wake kabla ya ndoa yetu. Baada ya kufunga ndoa, mama yake aliona kwamba nafasi yake imechukuliwa. Haikuwa rahisi kwake kukubali hilo.”
Huenda ikawa vigumu pia kwa baadhi ya wenzi wa ndoa wapya.James aliyenukuliwa mwanzoni anasema hivi: “Kuwa na wakwe si sawa na kuwa na marafiki unaochagua. Ni sawa na mtu fulani akuambie, ‘Umepata marafiki wawili wapya, iwe unapenda au la.’ Hata kama wanakuudhi bado ni sehemu ya familia yako!”

 UNACHOWEZA KUFANYA

Ikiwa wewe na mwenzi wako hamwelewani inapohusu jinsi ya kushughulika na wakwe, jitahidini kurekebisha tatizo hilo kwa pamoja. Fuateni ushauri huu wa Biblia: ‘Tafuteni amani, na kuifuatia.’—Zaburi 34:14.
Ili kufanya hivyo, fikiria hali zifuatazo. Kila hali inaonyesha mtazamo wa mume au mke. Hata hivyo, wote wawili wanakabili changamoto zilezile na kanuni zitakazoonyeshwa zinaweza kuwasaidia kushughulika na wakwe.
Mke wako anasema kwamba angefurahi ikiwa ungekuwa na uhusiano mzuri na mama yake. Lakini unaona ni vigumu kushughulika na mama yake.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mke wako kuhusu tatizo hilo na uwe tayari kufanya marekebisho. Jambo kuu si namna unavyohisi kuhusu mama-mkwe bali jinsi unavyohisi kuhusu mwenzi wako uliyeapa kwamba utampenda. Wakati wa mazungumzo mwambie njia moja au mbili hususa utakazotumia kuboresha uhusiano wako na mama yake na ujitahidi kufanya hivyo. Kadiri anavyoona jitihada zako, mke wako atakuheshimu zaidi.—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 10:24.
Mume wako anasema kwamba unawahangaikia zaidi wazazi wako kuliko yeye.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mume wako kuhusu tatizo hilo ili kujua maoni yake. Ni kweli kwamba mume wako hahitaji kuwa na hofu ya namna hiyo ikiwa unawaheshimu wazazi wako. (Methali 23:22) Hata hivyo, unahitaji kumhakikishia kupitia maneno na matendo yako kwamba bado unamthamini sana. Akiwa na uhakika huo, mume wako hatahisi kwamba anashindana na wazazi wako ili tu umthamini.—Kanuni ya Biblia: Waefeso 5:33.
Mke wako anaomba ushauri kwa wazazi wake badala ya kukuomba wewe.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mke wako na mkubaliane kuhusu mambo ambayo mnaweza kuomba ushauri wa wazazi. Jitahidi kuwa mwenye kukubali sababu. Je, mara zote ni vibaya kuongea na mzazi kuhusu tatizo fulani? Ni wakati gani unaofaa wa kuzungumza nao? Mkikubaliana kuweka mipaka yenye usawaziko, hali hiyo haitakuwa tatizo. —Kanuni ya Biblia: Wafilipi 4:5.
by : Unknown
Jambo muhimu la kufahamu ni kwamba agano la kale lilipatiwa taifa la Israeli wala sio wakristo. Baadhi ya sheria hizo zilikuwa za kuwafanya waisraeli wajue jinsi ya kumtii na kumfurahisha Mungu (amri kumi za Mungu kwa mfano), baadhi yazo zilikuwa zikiwafunza jinsi ya kumuabudu Mungu (kwa ile njia ya sadaka), nyengine zilikuwa za kuwafanya waisraeli wawe watu maalum (kama sheria za aina za mavazi na chakula). Hakuna sheria yoyote ya agano la kale inayotumika kwetu sasa. Yesu alipokufa msalabani, alimaliza matumizi ya sheria ya agano la kale (Warumi 10:4; Wagalatia 3:23-25; Waefeso 2:15).

Mahali pa sheria ya agano la kale, tuko chini ya sheria ya kristo (Wagalatia 6:2) ambayo ni, “Mpende bwana Mungu wako na moyo wako wote akili zako zote na nguvu zako zote. Hii ndiyo ya kwanza na amri iliyo kuu. na ya pili ni kama ya kwanza, mpende jirani yako kama nafsi yako. Torati yote na manabii inakamilishwa katika amri hizi mbili” (Mathayo 22:37 – 40). Tukifanya mambo haya mawili tutakuwa tunatimiza yale kristo angetaka tuyafanye, “na huu ndio upendo wa Mungu: kutii amri zake. Na amri zake si nzito” (waraka wa kwanza wa Yohana 5:3). Kwa mtazamo, amri kumi za Mungu hazina uhusiano na wakristo. Hata hivyo, tisa katika amri kumi za Mungu zimerudiwa katika agano jipya (zote isipokuwa ile ya kuweka sabato). Kwa kwaida kama tunampenda Mungu hatutakuwa na miungu miginemila yeye. Tukiwapenda majirani zetu hatutawaua, hatutawadanganya,hatutazini nao, wala kutamani kile walichonacho. Kwa hivyo hatuko chini ya sheria ya agano la kale. Sisi ni wakumpenda Mungu na pia majirani zetu. Tukifanya mambo haya mawili kwa uaminifu wa moyo, kila kitu kitakuwa sawa.
by : Unknown
 Biblia inazungumzia juu ya vitu hivi tulivyonavyo ili tushinde maisha yetu ya dhambi:

(1) Roho Mtakatifu – kipawa kimojachapo ambacho Mungu ametupa (kanisa lake) kwa ajili ya kuwa na ushindi katika maisha ya kikristo ndani ya Roho Mtakatifu. Mungu anatofautisha mtendo ya mwili na matunda ya Roho Mtakatifu katika wagalatia 5:16-25. katika andiko hilo tunashauriwa kutembea katika uwepo wa Roho Mtakatifu. “waumini wote tayari wamejazwa na Roho Mtakatifu”,lakini hapa tunasisitizwa kupatia nafasi Roho Mtakatifu atutawale na kutuongoza. Hii ina maana ya kuwa tusikilize sauti yake tusije tukatenda mapenzi yetu wenyewe.

Tofauti ambayo Roho Mtakatifu anaweza kuifanya maishani mwa mtu ni kama ile ya Petro, kabla hajajazwa Roho Mtakatifu alimkana Yesu mara tatu, na alikuwa mbeleni ameahidi kumfuata Yesu mpaka kwenye hatari ya kifo angekufa naye. Baada ya kujazwa na Roho alizungumza waziwazi na kwa ujasiri mbele ya wayahudi juu ya mwokozi katika siku ya pentekote.

Unatembea ndani ya Roho ukiwa humzuii anapotaka kujidhihirisha (“kumzima Roho” wathesalonike wa kwanza 5:19) na una kiu ya kujazwa naye kila wakati (Waefeso 5:18-21). Je mtu hujazwaje na Roho Mtakatifu? Kwanza ni kwa mapenzi ya Mungu kama vile ilivyo katika agano la kale. Alikuwa akichagua watu Fulani, kuwajaza kwa ajili ya kutekeleza kazi ama wadhifa Fulani (Mwanzo 41: 38; Kutoka 31:3; Hesabu 24:2; Samueli wa kwanza 10:10; na kadhalika.) Ninaamini kuwa kuna ushahidi katika Waefeso 5:18-21 na Wakolosai 3:16 yakuwa Mungu huchagua kujaza wale wanaojijaza Neno la Mungu kwa kuwa kote kote ni kujazwa uwezo wa Mungu.

(2) Neno la Mungu, Biblia – Timotheo wa pili 3:16-17 inasema ya kwamba Mungu ametupa neno lake ili lituandae katika kufanya kazi njema. Linatufundisha jinsi ya kuishi na cha kuamini, linatufunulia kama tumetenda makosa na kuturudisha katika njia ya sawa. Kama waebrania 4:12 inavyosema Neno la Mungu liko hai na lina nguvu ya kupenya ndani ya nafsi zetu kung’oa lile tatizo ambalo mwanadamu hangeweza kulitatua. Mwandishi wa zaburi azungumzia uwezo wa Neno la Mungu juu ya kubadilisha maisha ya watu katika zaburi 119:9,11,105 na aya nyengine. Joshua aliambiwa siri ya kushinda adui zake (inayoashiria pia vita vyetu vya kiroho) ni kwamba asilisahau Neno la Mungu bali alitafakari usiku na mchana ili akalitimize. Haya aliyatenda, ijapokuwa maagizo yenyewe hayakuwa na uhusiano na mambo ya kivita lakini yakampa ushindi katika vita vya kuimiliki nchi ya ahadi.

Hii ni sehemu ambayo mara nyingi tunaipuuza. Tunapenda kubeba biblia tukienda kanisani ama kusoma aya za kukariri lakini hatuyatilii maanani yale tuyasomayo. Hatuyatafutii nafasi maishani mwetu kiasi cha kutubu dhambi zetu na kumtukuza Mungu kwa kipawa hiki. Tunasoma tu kiasi cha kupata mtazamo Fulani juu ya wokovu lakini hatuongezi juhudi zozote katika kutafakari kwetu mara kwa mara kiasi cha kutufanya tuwe na afya nzuri kiroho.

Ni muhimu sana kwako ufanye tabia ya kusoma neno la Mungu. Kama bado hujazoea basi Roho anakusisitiza uwe na tabia ya kulisoma Neno la Mungu. Nina kushauri uwe na kumbukumbu ya yale uliyoyasoma kwa kuyanakili kwenye daftari lako au kwenye kompyuta. Biblia ndicho kifaa Roho hutumia katika maisha yetu na maisha yaw engine (Waefeso 6:17), ikiwa ni sehemu kubwa ya silaha mojawapo ambayo Mungu hutupa ili tupigane vita vya kiroho (Waefeso 6:12-18)!

(3) Maombi – Hii pia ni njia nyengine ambayo Mungu ametupatia. Njia hii wakristo wengi huitaja tu kwa maneno lakini hawaitumii. Tuna ibada za maombi na nyakati za maombi na kadhalika lakini hatuoni manufaa ya jambo hilo sawa na kanisa la kwanza (Matendo 3:1; 4:31; 6:4; 13:1-3, na kadhalika). Paulo mara kwa mara arudia kueleza vile alikuwa akiwaombea wale aliokuwa akiwahudumia. Lakini tunapokuwa peke yetu hatuitumii njiaa hii. Mungu ametuahidi mambo mazuri ya ajabu kuhusiana na maombi (Mathayo 7:7-11; Luka 18:1-8; Yohana 6:23-27; Yohana wa kwanza 5:14-15, na kadhalika.) Paulo analiongezea mkazo tena katika mafundisho yake juu ya kujiandaa kwa ajili ya vita vya kiroho (Waefeso 6:18)!

Je, ni muhimu kiasi gani njia hii? Tunapomtazama tena Petro, tunaona maneno ya kristo aliyomwambia kabla hajamkana kule Gethsemane. Yesu alipokuwa akiomba Petro alilala. Yesu akamwambia, “Kesheni mkiomba ili msiingie majaribuni: Roho inataka lakini mwili ni dhaifu” (Mathayo 26:41). Wewe pia kama Petro unataka kufanya mema lakini huna nguvu yakutosha kufanyia hayo. Lazima tufuate mausia ya Mungu, tuendelee kumtafuta, tukibisha na kumuuliza… na atatupatia nguvu ile tuitafutayo (Mathayo 7:7 na kuendelea). Lakini lazima tuitilie mkazo njia hii maishani mwetu ndiyo tufaulu. Sisemi ya kwamba maombi ndiyo njia maalum zaidi. La sivyo. Mungu ni wakutisha. Maombi ni kukubali hali zetu za udhaifu, ukuu wa Mungu mwenye nguvu na asiyeshindwa ili tupate uwezo huo huo tuweze kuyafanya yaliyo mapenzi yake (wala si yetu) (Yohana wa kwanza 5:14-15).

(4) Kanisa – Hii ni mojawapo ya njia tunazozifumbia jicho. Yesu alipowatuma wanafunzi wake aliwatuma wawili wawili (Mathayo 10:1). Tunaposoma juu ya habari za safari za wale wamishenari katika kitabu cha matendo ya mitume, hawakuenda mmoja mmoja bali katika makundi, wawili wawili au zaidi.Yesu alisema mahali wawili au watatu wamekusanyika kwa ajili ya jina langu, nami nitakuwa katikati yao (Mathayo 18:20). Anatuamuru tusiache kukusanyana pamoja kama kawaida za watu wengine zilivyo bali tuutumie wakati wa kuwa pamoja kwetu kwa kutiana moyo katika upendo na matendo mema (Waebrania 110:24-25). Anatuagiza kutubu dhambi zetu mmoja kwa mwingine (Yakobo 5:16). Katika habari za hekima katika agano la kale tunaambiwa ya kwamba chuma hunoa chuma mwenziwe, vivyo hivyo mtu huchangamsha sura ya rafiki yake (Methali 27:17) “kamba ya nyuzi tatu haikatiki rahisi.” “kuna nguvu katika umoja wa wengi (Mhubiri 4:11-12).

Baadhi ya watu ninaowafahamu wamepata kaka na dada katika kristo wanaotangamana pamoja au kwa simu na wanaelezana vile wanaendelea na maisha ndani ya kristo na wanawajibika katika kuombeana huku wakiishi maisha sawa na Neno la Mungu. Mabadiliko mara nyingine huja haraka na wakati mwengine polepole. Lakini Mungu ametuahidi ya kwamba kadri tunavyoendelea kutumia njia hizi alizotuwekea, ndivyo atatuletea mabadiliko maishani mwetu. Vumilia ukijua ya kuwa ni mwaminifu katika ahadi zake.
Posted on : [0] comments Label: ,

JEWEWE UNATOA FUNGU LA KUMI?

by : Unknown
Kutoa fungu la kumi ni jambo ambalo wakristo wengi hung’ang’ana nalo. Katika makanisa mengine kutoa fungu la kumi imesisitizwa kupita kiasi. Wakristo wengi pia hukataa kutii agizo la kutoa sadaka kwa Bwana. Kutoa fungu la kumi au sadaka inahitajika kuwa ni kitendo cha furaha na baraka. Lakini sivyo katika makanisa ya sasa.

Kutoa fungu la kumi ni agizo la agano la kale. Hili lilikuwa sharti la kila mwenye kupata zao au mfugo alete sehemu ya kumi ya pato hekaluni (mambo ya walawi 27:30; hesabu 18:26; kumbukumbu la torati 14;24; mambo ya nyakati ya pili 31:5). Wengine huchukulia ya kuwa fungu la kumi, katika agano la kale ilikuwa kama sehemu ya ushuru uliokuwa ukitolewa kwa ajili ya makuhani na walawi. Agano jipya haiamrishi wala kupendekeza mfumo halali wa kutolea fungu la kumi. Paulo asisitiza kuwa waumini watenge sehemu ya mapato yao kwa ajili ya kusimamia kanisa (wakorintho wa kwanza 16:1-2).

Agano jipya halielezi kiasi cha pato ambacho ni kitengwe kwa ajili ya kusimamia kanisa. (wakorintho wa kwanza 16:2). Kanisa la kikristo leo limechukua kile kiwango cha fungu la kumi kutoka kwa agano la kale na kukisisitiza kuwa ndicho kiwango cha chini cha mkristo kutoa. ijapokuwa agano jipya haitoi kiwango cha kutoa, inaelezea umuhimu na manufaa ya kutoa. Ni watoe sawa na uwezo wao “ kulengana na pato lake.” Wakati mwingine ina maana ya kutoa zaidi ya fungu la kumi, na mara nyingine kichache kuliko fungu la kumi. Yote hutegemea uwezo wa mkristo mwenyewe na mahitaji ya kanisa. Kila mkristo sharti aombe na kutafuta hekima kutoka kwa Mungu juu ya swala hili (Yakobo 1:5). “ kila mtu niatoe kile alicho azimia kutoa kutoka ndani ya moyo wake, si kwa manung’uniko wala kulazimishwa, kwa kuwa Mungu hupenda kwenye kutoa kwa moyo mkunjufu” (wakorintho wa pili 9:7).