Latest News


More

JINSI KIJANA ANAVYOWEZA KUFANIKIWA AKIWA SHULENI

Posted by : Unknown on : Saturday, September 13, 2014 0 comments
Unknown
Saved under :


Fanya Mambo kwa Utaratibu


Unahitaji tu jitihada kidogo ili kupanga mambo kwa utaratibu, lakini unaweza kupata faida nyingi kama vile, kuokoa wakati, kutokuwa na mkazo sana, na kupata alama za juu.
WAZIA umeenda dukani kununua kitu fulani, lakini bidhaa zote zimewekwa ovyoovyo bila mpangilio wowote. Utatumia muda gani kupata kitu unachotaka? Je, haingekuwa rahisi kukipata ikiwa bidhaa zingekuwa zimepangwa kwa utaratibu na vijia vyote vya duka hilo viwe na vibandiko vinavyoonekana waziwazi? Unaweza kutumia utaratibu huohuo kuhusu mambo yako ya shule. Jinsi gani?

Panga ratiba.

“Pindi moja nilisahau kabisa kufanya kazi zangu za shuleni na pia nikasahau kufanya kazi nilizopewa nyumbani kwa sababu nilienda kumtembelea rafiki yangu mwisho juma wote,” anasema Zachary, mwenye umri wa miaka 18, anayeishi Marekani. “Jumatatu, niliwasihi sana walimu wangu wanipe muda wa kumaliza kazi zangu za shule. Sasa mimi huandika orodha ya mambo ya kufanya ili niyakumbuke.”
Kuandika orodha ya mambo ya kufanya pia kumemsaidia Celestine, mwanamke anayeishi Papua New Guinea. Anasema hivi kuhusu wakati alipokuwa shuleni: “Niliandika ratiba ya utendaji wangu wote, kutia ndani kazi za shule, mitihani, na tafrija. Kufanya hivyo kulinisaidia kujua mambo ya kutanguliza na kufanya mambo kwa wakati.”
Dokezo: Andika mambo unayotaka kufanya kwenye kijitabu kidogo, au kwenye simu yako ya mkononi au kifaa kingine cha kielektroniki.

Usiahirishe.

Ni rahisi kusema, “Nitafanya jambo hilo baadaye.” Ni afadhali kufanya mambo mapema iwezekanavyo—hasa kazi za shule.
Dokezo: Uwe na zoea la kufanya kazi za shule mara tu ufikapo nyumbani, kabla ya kuwasha televisheni au kujihusisha katika burudani nyingine yoyote.

Panga vifaa vyako vya shule.

Umewahi kufika shuleni na kugundua kwamba umesahau kitabu au kalamu? Unaweza kuepuka tatizo hilo. Jinsi gani? “Sikuzote mimi huweka vifaa vyangu vya shule kwenye mkoba wangu mapema,” anasema Aung Myo Myat, kijana anayeishi Myanmar.
Dokezo: Weka mkoba wako wa shule ukiwa nadhifu na panga vitu kwa utaratibu ili iwe rahisi kupata kitu unachotaka.
Jambo kuu: Kufanya mambo kwa utaratibu kutakusaidia usisahau vitu, usichelewe, na uwe na wakati wa kutosha wa kufanya mambo mengine yaliyo muhimu.
Anza sasa! Fikiria sehemu ambayo wewe unahitaji kuwa na utaratibu. Kisha mwombe mzazi au rafiki madokezo ya jinsi ya kuboresha sehemu hiyo.
(Source: http://www.jw.org)

No comments:

Leave a Reply