Latest News


More

BIBLIA INARUHUSU KUJICHANJA CHALE?

Posted by : Unknown on : Thursday, April 23, 2015 0 comments
Unknown
Saved under :

Jibu la Biblia

Biblia inataja kuhusu kuchanja chale mara moja tu katika kitabu cha Mambo ya Walawi 19:28, ambapo tunasoma hivi: “Msijitie alama ya chanjo.” Mungu aliwapa Waisraeli amri hiyo, na hivyo kuwafanya tofauti na watu waliowazunguka ambao walijitia alama za majina au maumbo ya miungu yao mwilini. (Kumbukumbu la Torati 14:2) Ingawa Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli haiwahusu Wakristo, tunapaswa kuzingatia kanuni inayotegemea sheria hiyo.

Je, Mkristo anapaswa kuchanja chale au kuuchora mwili wake?

Maandiko yafuatayo yanaweza kukusaidia ujue jinsi ya kutenda:
  • “Wajipambe kwa mavazi yenye . . . kiasi.”—1 Timotheo 2:9 New World Translation) Kanuni hiyo inawahusu wanaume na wanawake. Tunapaswa kuheshimu hisia za wengine na kuepuka kujifikiria wenyewe.
  • Wengine wanataka watambuliwe na watu au waonekane wako huru, ilhali wengine wanajichanja chale ili waonyeshe kwamba wanajiamini. Hata hivyo, Biblia inawatia moyo Wakristo ‘watoe miili yao kuwa dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zao za kufikiri.’ (Waroma 12:1) Tumia ‘nguvu zako za kufikiri’ kuamua ni kwa nini unataka kujichanja chale. Ikiwa unafanya hivyo kwa sababu unataka kufuata mtindo fulani au kuonyesha kwamba wewe ni mshiriki wa kikundi fulani, kumbuka kwamba kujichanja chale kuna madhara ya kudumu. Kuchunguza nia yako kunaweza kukusaidia kufanya uamuzi wa hekima.—Methali 4:7.
  • “Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta faida, lakini kila mtu anayetenda haraka-haraka bila shaka huuelekea uhitaji.” (Methali 21:5) Mara nyingi uamuzi wa kujichanja chale hufanywa bila kufikiria kwa uzito, na unaweza kuathiri uhusiano wako na wengine au kazi. Ni ghali sana kuchanja chale na kuna maumivu mengi sana unapoamua kuziondoa. Utafiti—kutia ndani biashara iliyositawi ya kuondoa watu chale—inaonyesha kwamba idadi kubwa ya watu waliojichanja chale wanajuta ni kwa nini walifanya hivyo.

No comments:

Leave a Reply