Latest News


More

JE MUNGU YUKO KARIBU AU MBALI NAWE?

Posted by : Unknown on : Wednesday, October 1, 2014 0 comments
Unknown
Saved under :

 

Mtu anayetafakari kumhusu Mungu
 

Je, Unahisi Mungu Yuko Karibu na Wewe?

“Kuwa na uhusiano mzuri na Mungu kunakufanya uhisi usalama, utulivu, na amani. Unahisi kwamba Mungu anakutakia mema siku zote.”—CHRISTOPHER, MWANAMUME KIJANA NCHINI GHANA.
“Mungu hukuona unapoteseka, naye anakupenda kuliko unavyoweza kuwazia.” —HANNAH, MSICHANA MWENYE UMRI WA MIAKA 13, ALASKA, MAREKANI.
“Inafariji na kufurahisha sana kutambua kwamba una uhusiano mzuri na Mungu!”—GINA, MWANAMKE KUTOKA JAMAIKA MWENYE UMRI WA MIAKA 40 HIVI.
Watu wengi huhisi kama Christopher, Hannah, na Gina. Wanaamini kwamba Mungu ni rafiki yao. Vipi wewe? Je, unahisi kwamba uko karibu na Mungu? Au, je, unataka kumkaribia au kuboresha uhusiano wako na Mungu? Huenda ukajiuliza hivi: ‘Inawezekanaje mwanadamu awe na uhusiano mzuri na Mungu Mweza-Yote? Ikiwa inawezekana, jinsi gani?’

INAWEZEKANA KUMKARIBIA MUNGU

Biblia inasema kwamba inawezekana kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Pia inasema kwamba Mungu alimwita Abrahamu, aliyekuwa Mwebrania ‘rafiki yake.’ (Isaya 41:8) Pia kumbuka mwaliko unaotolewa kwenye andiko la Yakobo 4:8: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” Kwa hiyo, ni wazi kwamba inawezekana kuwa na uhusiano mzuri au urafiki na Mungu. Lakini kwa sababu hatuwezi kumwona Mungu, inawezekanaje ‘kumkaribia’ na kuwa na uhusiano mzuri pamoja naye?
Ili kupata jibu la swali hilo, fikiria jinsi urafiki kati ya wanadamu unavyositawishwa. Kwa kawaida, watu hujuana majina na kisha kuanzisha urafiki. Halafu, kadiri wanavyoendelea kuwasiliana ndivyo urafiki wao unavyositawi. Urafiki wao huzidi kuimarika wanapoendelea kutendeana mambo mema. Ndivyo ilivyo pia tunapotaka kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Acheni tuchunguze jinsi ya kufanya hivyo.

No comments:

Leave a Reply