Latest News


More

HARUSI YA CUTHBERT NA MATILDA

Posted by : Unknown on : Wednesday, August 24, 2011 0 comments
Unknown
Saved under : ,
Ilikua ni siku ya furaha nderemo na chereko kwa Cuthbert Noah na Matilda Elias pale walipoamua kufunga pingu za maisha.
Cuthbert ambaye ni mwajiriwa katika kampuni ya Vodacom aliamua kuuaga ukapera na kufunga pingu za maisha katika kanisa la K.K.K.T Kinondoni Hananasif na Matilda Elias na baadaye tafrija iliyofanyika katika ukumbi wa Mamba Club ulioko Kinondoni.

Pichani ni Bwana na Bibi harusi wakiwa katika ufukwe wa hoteli ya Golden Tulip walikoenda kupiga picha mara baada ya kufunga pingu za maisha

Bwana harusi akifanya utambulisho wa ndugu katika ukumbi wa Mamba Club



Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ambaye pia ni mjomba wa bwana harusi Ndg Kichila akiwakaribisha wageni ukumbini

Mc wa sherehe hiyo akisherehesha katika Ukumbi wa Mamba Club Kinondoni siku hiyo


Maharusi wakiwa na wapambe wao katika ufukwe wa Golden Tulip Hotel.Katikai aliyevaa shati jekundu ni meneja wa hoteli hiyo ndugu Neel


Maharusi wakiwa na Junior (Cuthbert)


Maharusi wakiwa kwenye pozi kwenye hoteli ya Golden Tulip






Bwana harusi, msimamizi wake na mdau wa blog hii ndugu Kichila

Bwana harusi akiwa kwenye pozi

Bwana na bibi harusi




Maharusi wakiwa na baadhi ya ndugu zao kwenye ufukwe wa Golden Tulip
















Bibi harusi akisaini cheti mara baada ya kufunga pingu za maisha kwenye kanisa la K.K.K.T Usharika wa Hananasif


Bwana harusi nae akisaini cheti cha harusi


Maharusi wakipongezana mara baada ya kufunga pingu za maisha

Bibi harusi akila kiapo kanisani mbele ya mchungaji



Bwana harusi akimvisha pete bibi harusi


Maharusi wakiwa kanisani wakisikiliza mahubiri



Maharusi na wapambe wao mara baada ya kukabidhiwa vyeti vyao






Maharusi wakiwa na vyeti vyao mara baada ya kukabidhiwa na mchungaji




Junior naye alikuwepo

Tunaomba radhi wadau baadhi ya picha sio nzuri sana kutokana na kigugumizi cha mpigaji
Saved under : ,