Latest News


More

JE TUNAWEZA KUJUA NI NANI ALIANDIKA BIBLIA?

Posted by : Unknown on : Monday, September 16, 2013 0 comments
Unknown
Saved under :

Jibu la Biblia

Watu wengi wameambiwa kwamba hatuwezi kuwa na uhakika kuhusu mtu aliyeandika Biblia. Lakini mara nyingi Biblia inaonyesha wazi watu walioiandika. Sehemu fulani zinaanza kwa maneno kama vile “maneno ya Nehemia,” “maono ya Isaya,” na “neno la Yehova lililomjia Yoeli.”—Nehemia 1:1; Isaya 1:1; Yoeli 1:1.

Waandikaji wengi wa Biblia walikubali kwamba waliandika katika jina la Yehova, Mungu wa pekee wa kweli, na kwamba waliongozwa naye. Manabii walioandika Maandiko ya Kiebrania walitangaza hivi zaidi ya mara 300: “Yehova amesema hivi.” (Amosi 1:3; Mika 2:3; Nahumu 1:12) Waandikaji wengine walipokea ujumbe wa Mungu kupitia malaika.—Zekaria 1:7, 9.

Biblia iliandikwa na wanaume 40 hivi kwa kipindi cha miaka 1,600. Wanaume fulani walitumiwa kuandika zaidi ya kitabu kimoja cha Biblia. Kwa kweli, Biblia ni maktaba ndogo yenye vitabu 66. Ina vitabu 39 vya Maandiko ya Kiebrania, ambavyo kwa kawaida huitwa Agano la Kale, na vitabu 27 vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, ambavyo mara nyingi huitwa Agano Jipya.

No comments:

Leave a Reply