Latest News


More

UTAJUAJE KARAMA YAKO YA ROHO MTAKATIFU?

Posted by : Unknown on : Friday, October 11, 2013 0 comments
Unknown
Saved under :
Swali: "Ninawezaje kujua karama yangu ya Roho Mtakatifu?"
Jibu: Hakuna muujiza wa kiuganga ama jaribio sahihi ambalo laweza eleza kamili karama yetu ya Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu watupa vipawa vile apendavyo (1Wakorintho 12:7-11). Shida moja kwa Wakristo wote ni jaribio la kudumu katika sehemu yetu ya kipawa, ndio njia pekee tutaweza kumfanyia Mungu kazi katika sehemu zetu tunajihisi tumepewa kipawa. Mungu anatuita kwa unyenyekevu tumtumikie katika mambo yote. Atatuamini kwa kila kipawa au vipawa tunavyovihitaji kukamilisha jukumu ambalo ametuitia.

Kutambua sehemu zetu za kipawa twaweza kamilishwa katika njia mbali mbali. Vipawa vya Roho Mtakatifu hujaribi au hugundua, bali si kutegemewa kwa kila kitu, laweza kwa kweli kutusaidia kuelewa ni wapi sehemu zetu za kipawa. Thibitisho kutoka kwa wengine pia latupa mwangaza kuhusu vipawa vyetu vya Roho Mtakatifu. Watu wengine wanaotuona tukimtumikia Mungu, kila mara wanaweza kutambua kipawa cha Roho Mtakatifu ndani yetu  ambacho sisi wenyewe tunakipuuza au kukosa kukitambua. Maombi pia ni muhimu. Mtu mmoja ambaye anajua kamili vile tumepewa vipawa vya Roho Mtakatifu ni mtoaji wa vipawa mwenye-Roho Mtakatifu. Tunaweza kumuuliza Mungu atuonyeshe jinsi tumepewa kipawa kwa ajili ya utukufu wake.
Naam, Mungu anawaita wengine kuwa walimu na kuwapa kipawa cha ualimu. Mungu anawaita wengine kuwa watumishi na kuwapa kipawa cha kusaidia. Ingawa kujua kamili kipawa chetu cha Roho Mtakatifu haitupi ruhusa ya kutomfanyia Mungu kazi sehemu zilizo nje ya vipawa vyetu. Je! Ni muhimu kujua kipawa chako ambacho  Mungu amekupa? Naam. Je! ni makosa kuangazia kipawa sana kiwango tunakosa sehemu zingine tunaweza kumfanyia Mungu kazi? Naamu. Kama tumelazimishwa kumtumikia Mungu, atatupa vipawa vya Roho Mtakatifu tunavyovihitaji

No comments:

Leave a Reply