Latest News


More

PAPA FRANCIS AOMBA AMANI ISRAEL

Posted by : Unknown on : Wednesday, July 2, 2014 0 comments
Unknown
 Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa francis
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani papa francis ameutaja mzozo kati ya Palestina na Israel kama usiokubalika huku akizitaka pande zote mbili kufanya maamuzi ya busara ili kuweka amani.
Akizungumza mjini Bethlehem ,papa Francis ametaka kubuniwa kwa taifa huru la Palestina pamoja na Israel.
Aidha alifanya maombi katika eneo ambalo Yesu anadaiwa kuzaliwa.

Akiwa katika ziara yake ya mji wa Bethlehem ,kiongozi huyo wa dini alisimama katika eneo ambalo Israel inajenga ukuta mkubwa pamoja na eneo la West bank ili kufanya maombi.
Maandishi yaliokuwa juu yake alipokuwa akiomba yalisema 'papa tunamtaka mtu atakayezungumzia kuhusu haki'.

No comments:

Leave a Reply