Latest News


More

Serikali yasema hakuna Ebola Tanzania

Posted by : Unknown on : Friday, August 15, 2014 0 comments
Unknown
Saved under :
Serikali ya Tanzania yathibitisha kutokuwepo kwa ugonjwa huo

Tanzania imesema haina mgonjwa aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola.
Kauli hiyo inakuja baada ya kufanyiwa uchunguzi kwa wagonjwa wawili waliotiliwa shaka kuwa na ugonjwa huo.
Waziri wa Afya wa Tanzania Seif Rashid ameiambia BBC, wagonjwa hao waliohisiwa kupata maambukizo kutokana na dalili za awali, ni wa kutoka Benin na Mtanzania, lakini vipimo vimeonesha hawana maambukizo hayo.
Amesema tayari eneo maalumu limetengwa kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wagonjwa wanaotiliwa shaka kuwa na ugonjwa huo.
Mafunzo yametolewa pia kwa wataalamu watakao hudumia wagonjwa iwapo watatokea.
Vifaa maalumu vitakavyotumiwa na watoa huduma katika kuhudumia wagonjwa, vimewekwa pia.

Wizara ya Afya ya Tanzania inaongeza uwezo wa kufanya uchunguzi, katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, ambao wasafiri wengi kutoka nje huutumia.

No comments:

Leave a Reply