Latest News


More

KWA NINI TUSALI UFALME WA MUNGU UJE?

Posted by : Unknown on : Wednesday, October 1, 2014 0 comments
Unknown
Saved under :

Kwa nini tusali Ufalme wa Mungu uje?

Yesu Kristo akienda kushinda adui za Ufalme wa Mungu
Je, ungependa kujua mengi kuhusu Ufalme wa Mungu na mambo utakayotimiza?


Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni. Yesu aliwaambia wafuasi wake wasali uje kwa sababu, utarudisha uadilifu na amani duniani. Hakuna serikali ya wanadamu inayoweza kuondoa kabisa jeuri, magonjwa, au ukosefu wa haki, lakini Ufalme wa Mungu unaweza na utafanya hivyo. Mungu amemchagua Mwana wake Yesu, awe Mfalme wa Ufalme huo. Yehova pia amewachagua baadhi ya wafuasi wa Yesu watawale pamoja na Yesu katika Ufalme huo.—Soma Luka 11:2; 22:28-30.
Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utawaangamiza wote wanaopinga utawala wa Mungu. Hivyo, tunaposali Ufalme wa Mungu uje, tunaomba serikali ya Mungu ichukue mahali pa serikali zote za wanadamu.—Soma Danieli 7:13, 14; Ufunuo 11:15, 18.

Kwa nini Ufalme wa Mungu utawanufaisha watu?

Yesu ni Mfalme anayefaa kwa sababu ana huruma. Akiwa Mwana wa Mungu, pia ana nguvu za kuwasaidia wote wanaomlilia Mungu awasaidie.—Soma Zaburi 72:8, 12-14.
Ufalme wa Mungu utawanufaisha wote wanaosali kwa unyoofu uje na wanaoishi kulingana na mapenzi ya Mungu. Hutajuta kamwe ukijifunza yale ambayo Biblia inasema kuhusu Ufalme wa Mungu!—Soma Luka 18:16, 17; Yohana 4:23.
(Source: www.jw.org)

No comments:

Leave a Reply