Written by Anonymous

HAPPY NEW YEAR 2015

by Anonymous / 06 Jan 2015

...

Written by Anonymous

MERY CHRISTMAS

by Anonymous / 25 Dec 2014

WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRIS...

Written by Anonymous

HAMUGEMBE PRAISE AND WORSHIP TEAM KUZINDUA ALBUM YAO MWEZI APRIL

by Anonymous / 31 Mar 2014

 Kikundi cha Hamugembe Praise and Worship Team cha mjini Bukoba  kinatarajia kuzindua album yao ya nyimbo za kusifu na kuabudu ...

Written by Anonymous

WE WISH YOU A HAPPY NEW YEAR 2014

by Anonymous / 31 Dec 2013

Leo ndio siku ya mwisho kwa mwaka huu 2013 na masaa machache yajayo tutaingia mwaka ujao 2014.Mtandao huu unawatakia kila la kheri na ba...

Written by Anonymous

KWAYA KUU YA USHARIKA WA AZANIA FRONT NDIO MABINGWA WA UIMBAJI WA K.K.K.T – DMP

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

Written by Anonymous

MASHINDANO YA UIMBAJI KWAYA KUU NGAZI YA DAYOSISI YA KANISA LA K.K.K.T (DMP) YAFANA USHARIKA WA MBEZI BEACH LEO

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

KUTOKA MADHABAHUNI

IBADA KATIKA KANISA LA LIVING WATER CENTER MAKUTI KAWE JUMAPILI HII

Jumapili hii ilifanyoka ibada nzuri katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe ambapo kiongozi wa kanisa hilo Mtume Onesmo Ndegi  (pichani juu) aliongoza na kuhubiri Pichani juu Mtume Onesmo Ndegi akimtambulisha ndugu wa m...

More KUTOKA MADHABAHUNI
More NENO LA LEO
More MAHUBIRI
More MAOMBI

HABARI ZA KIDINI

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MHESHIMIWA MAKONDA AZINDUA VITABU VYA INJILI KANISA LA LIVING WATER CENTER KAWE KAWE

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mheshimiwa Paul Makonda jumapili hii alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa vitabu vya injili vya mwalimu Lilian Ndegi katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe Bwana Makonda (pichani juu) alimsh...

More HABARI ZA KIDINI

More HABARI ZA KIDINI

ASKOFU MALASUSA AONGOZA HARAMBEE KUBWA KATIKA USHARIKA WA K.K.K.T MAGOMENI MVIRINGO

Posted by : Unknown on : Monday, May 13, 2013 0 comments
Unknown
 Siku ya jumapili tarehe 12/05/2013 ilifanyika harambee kubwa ya ujenzi wa kanisa katika Usharika wa K.K.K.T Magomeni mviringo.Katika ibada hiyo ambayo ilitanguliwa na uwekaji wa jiwe la msingi wa kanisa hilo jipya iliongozwa na mkuu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  ambaye pia ni Askofu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dr Alex Gerhaz Malasusa

Ibada hiyoiliyokuwa na waumini wengi  ilihudhuriwa pia  na viongozi takribani wote wa Dayosisi hiyo na wachungaji wa sharika mbalimbali ilitanguliwa na maandamano ya wanakwaya na wachungaji wakiongozwa na kwaya ya matarumbeta ya Usharika wa Wazo Hill


Picha ya juu Mgeni rasmi Askofu Dr.Alex  Gerhaz Malasusa akiwa kwenye maandamano tayari kwenda kuweka jiwe la msingi la kanisa hilo.Aliyeongozana naye pembeni ni mchungaji toka Marekani
 Askofu Dr Alex Gerhaz Malasusa akiongoza ibada ya kuweka jiwe la msingi.Aliyeko mbele kulia ni mchungaji kiongozi wa Usharika wa Magomeni Mchungaji Henry Mwinuka.Nyuma ya mchungaji Mwinuka ni mwenyekiti wa kamati ya ujenzi engineer Angaufoon Nkya

 Askofu Dr Alex Gerhaz Malasusa akikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la  msingi wa kanisa hilo la Usharika wa  Magomeni



 Wanakwaya wa kwaya kuu ya Msasani wakiimba katika ibada hiyo


 Kwaya ya watoto wa Usharika wa Magomeni wakiimba katika ibada hiyo ya harambee
Askofu Dr Alex Gerhaz   Malasusa ambaye pia alikuwa mgeni rasmi akiendesha ibada.



 Waumini na wageni mbalimbali wakifuatilia ibada hiyo kwa makini.
 Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa mbele na Askofu Dr Alex Gerhaz Malasusa.Mbele kabisa ni mheshimiwa Philip Mangula (makamu mwenyekiti wa CCM Bara) akiwa na mke wake  wakitoa ahadi yao.Aliyeko kushoto kwake  (mwenye miwani) ni mkuu wa majeshi nchini General Davis Mwamunyange

Mke wa mchungaji toka Marekani akitoa sadaka katika ibada hiyo.Nyuma yake ni mke wa Askofu wa K.K.K.T Dr Alex Gerhaz Malasusa.Pembeni aliyesimama ni mzee wa kanisa la Usharika wa Magomeni ambaye pia alikua mwenyekiti wa kamati ya kumbukumbu ya harambee hiyo Mzee James Mushi.

 Juu na chini ni baadhi ya waumini wakifuatilia ibada hiyo kwa makini

 Washarika na wageni mbalimbali wakiwa watulivu wakifuatilia ibada hiyo ya harambee.
 Ibada hiyo ilihudhuriwa pia na waandishi mbalimbali wa vyombo vya habari wakiwepo wa Upendo Fm Redio ambao walikua wakirusha ibada hiyo moja kwa moja (live) kama wanavyoonekana pichani juu.
 Katibu wa baraza ndugu Elius Mziray  akisoma risala ya  maendeleo ya ujenzi ulikofikia mpaka sasa .Ujenzi wa Nyumba hiyo ya ibada kwa mujibu wa maelezo ya katibu huyo unategemewa kutumia kiasi  cha shilingi bilioni 2.Mpaka sasa  ujenzi umeshatumia kiasi cha shilingi milioni 500.

Katibu huyo alisema jengo hilo la kumwabudu Mungu likikamilika linatazamiwa kuchukua waumini 1800, likiwa na vyumba vya ofisi 4, vyumba vya mikutano/semina 4, vyenye uwezo wa kuchukua watu 60 hivi kila kimoja

 Wanakwaya wa Magomeni wakiimba katika ibada hiyo.Wanakwaya hawa waliimba wimbo uliokuwa unahimiza watu kujenga nyumba ya Bwana.


 Mkuu wa majeshi  General Davis Mwamunyange akitoa ahadi yake siku hiyo ya harambee mbele ya Askofu Dr Alex Gerhaz  Malasusa


 Mkuu wa majeshi  General  Mwamunyange akiwa ameshika saa kubwa yenye picha ya kanisa jipya ambayo ilinadiwa siku hiyo ya mnada


Mchungaji wa Usharika wa Magomeni Mviringo mchungaji Henry Mwinuka  akiwashukuru waumini pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria katika ibada hiyo.Katika ibada hiyo ya harambee kiasi cha shilingi milioni  160 zilipatikana ikiwa ni fedha taslim pamoja na ahadi mbalimbali.

Ulinzi uliimarishwa sana katika maeneo ya kanisa.Pichani askari wa jeshi la polisi wakiwa wanapata chakula mara baada ya kazi ya harambee kukamilika.
Mungu awabariki wote waliofanikisha harambee hiyo

No comments:

Leave a Reply