Latest News


More

RAIS OBAMA AMALIZA ZIARA YAKE NCHINI TANZANIA

Posted by : Unknown on : Wednesday, July 3, 2013 0 comments
Unknown
Saved under : ,
 Hatimaye rais Baraka Obama wa Marekani amemaliza ziara yake nchini Tanzania na kurudi nchini mwake Marekani
Katika ziara yake hiyo ya siku mbili ya  kiserikali pamoja na mambo mengine alizungumzia kuhusu jinsi Marekani itakavyosaidia Afrika kupata umeme wa uhakika
 Pichani rais Kikwete pamoja na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na balozi wa Marekani nchini Tanzania wakimpungia rais Obama mara baada ya kupanda kwenye ndege yake jana
 Kabla ya kuondoka uwanjani alipata nafasi ya kuagana na viongozi mbalimbali wa serikali .Pichani akiagana na meya wa  jiji la Dar es salaam huku meya wa Ilala na balozi wa Tanzania nchini Marekani balozi Liberata Mulamula wakisubiri zamu zao
 Awali kabla ya kuondoka Rais Obama alipata nafasi ya kupigiwa wmbo wa taifa wa nchi yake pamoja na wimbo wa taifa la  Tanzania .Pichani akipokea saluti wakati zikipigwa nyimbo hizo

Kabla ya hapo rais Obama alipata nafasi asubuhi ya kukagua mitambo ya kufua umeme ya Symbion ambayo ni ya wawekezaji toka nchini Marekani.Pichani juu akitoa maneno machache wakati akiwa  kwenye eneo la mitambo hiyo Ubungo
 Rais Obama akionyesha ujuzi wa kucheza na mpira unaoweza kufua umeme
 Rais Kikwete na mwenyeji wake rais  Obama wakipata maelezo ya mpira unaoweza kufua umeme toka kwa mtaalam
Rais Kikwete akicheza mpira maaluma ambao unajaa nishati kila unapochezwa hivyo kutumiwa kuchajia simu au kuwasha taa kwenye eneo la mitambo ya Symbion jana

No comments:

Leave a Reply