Latest News


More

SIKU YA FAMILIA USHARIKA WA MWENGE (K.K.K.T) YAFANA

Posted by : Unknown on : Monday, July 1, 2013 0 comments
Unknown



Usharika wa Mwenge wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani (K.K.K.T) umefanya siku maalum ya familia lengu likiwa ni kukutanisha wazazi na watoto ili kumwabudu Mungu kwa pamoja

Tukio hilo kubwa lilifanyika usharikani hapo likiwa limeandaliwa wamati huu ambao wanafunzi wengi wako likozo ili kuhakikisha kuwa wanasherehekea siki hiyo pamoja na wazazi wao .

Akizungumza wakati wa ibada hiyo Mchungaji kiongozi wa Usharika wa Mwenge Mchungaji Kaanasia Msangi (aliyeko kwenye picha ya juu) alisema wakati huu ambao kanisa linaadhimisha miaka 50 ya kuanzishwa kwake, kanisa linasisitiza umoja ndio maana nao wameona ni vyema kukutana na familia za Usharika huo ili kuendeleza umoja huo
Alisema kuna baadhi ya familia ambazo hufanya matembezi kwenye maeneo ambayo hayampi Mungu utukufu, hivyo imefika wakati sasa kubadilisha mtazamo na kukutana na familia kanisani ili kusherehekea kwa pamoja kwa kumsifu Mungu


Mwalimu akifundisha kwa msisitizo kundi la wanafamilia .Kundi hili lilikua linajumuisha familia ya mke na mume
 Familia mbalimbali zilikiaa pamoja kama mme na mke na kupata mafundisho ya ndoa na familia




Mwalimu wa kwaya ya Vijana mwalimu Mushi akiwa kwenye semina hiyo


Dr Eliwaza akiwa na mume wake kwenye semina hiyo ya family day


Bwana Mushi na mke wake nao wakifuatilia semina hiyo kwa makini

Bwana Urio na mke wake wakifurahia semina hiyo ya neno la Mungu



Mwinjilisti Mwigune akifundisha kwenye semina hiyo



Mzee Severe na mke wake nao wakifuatilia semina hiyo




Bwana na Bi somi wakifuatilia semina hiyo





 Baadhi ya wana kamati wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mchunhgaji wa Usharika huo wa Mwenge Mchungaji Kaanasia Msangi.Kutoka kushoto Mwinjilisti Mwigune, binti wa mchungaji. mchungaji Kaanasia na Mzee Godilisten Lema






Evelyne Kichila akiwa na dada yake wakipata chakula cha mchana kanisani siku hiyo

 Wanandoa walipata pia nafasi ya kukumbushia siku walipofunga ndoa.Hakika ilikua siku ya kukumbukwa usharikani hapo


Tukio hilo kubwa na la kihistoria liliwakutanisha wanafamilia mbalimbali wa Mwenge ambapo waliimba pamoja, kula pampja na watoto pia walipata nafasi ya kucheza pamoja

Akizungumza na mtandao huu wa Tumainiletu mara baada ya kumalizika kwa sherehe hiyo mmoja wa wajumbe wa kamati ya maandalizi ya siki hiyo ya Family Day ndugu Godilisten Lema alisema hakika Mungu ameonekana katika siku hiyo.Kulikuwepo na makundi mbalimbali ambayo yalipata mafundisho ya kipekee kama vile wajane, wagane, wazee, watoto, vijana nk.Walikiwepo waalimu mbalimbali walioandaliwa kwa ajili ya kufundisha masomo mbalimbali.

Mzee Lema Kulia (mmojawapo wa wanakamati ya maandalizi ya family day) akiwa na mwinjilisti wa Usharika Mwigune

 Mzee wa kanisa mama Chacha naye alikuwepo kwenye semina hiyo ya family day
 Mzee wa kanisa mama Palangyo naye alikuwepo siku hiyo ya family day
 Picha ya pamoja ya baadhi ya wanafamilia na wakufunzi wa semina hiyo
Mchungaji kiongozi wa Usharika wa Mwenge Mchungaji Kaanasia Msangi mara baada ya semina hiyo ya aina yake.



Siku hiyo kulikua na Ibada moja tu ambayo ilianza saa moja asubuhi na ilipofika saa tatu waumini walipata chai kwa pamoja kasha wakajigawa kwenye makundi mbalimbali kama vile Vijana, wajane , wagane, wazee, wanandoa wa kundi la kati, wakina mama nk.
Katika makundi hayo kulikua na waalimu waliofundisha masomo mbalimbali.Ilikofika mchana walipumzika kwa kupata chakula cha mchana kasha wakarudi tena kwa makundi tofauti na waalimu tofauti.Baada ya masomo hayo jioni walikutanika tena kwa pamoja kasha wakafanya maombi ya pamoja na kufunga sherehe hiyo , alisema ndugu Lema

No comments:

Leave a Reply