Latest News


More

UHURU WA MRISTO

Posted by : Unknown on : Tuesday, September 24, 2013 0 comments
Unknown
Saved under :




UHURU WA MKRISTO


Jumapili hii ilifanyika ibada nzuri katika Usharika wa K.K.K.T – Mwenge

Katika ibada hiyo iliyoongozwa na Mchungaji wa Usharika huo Mchungaji Kaanasia Msangi na mahubiri yaliongozwa na Mwinjilisti wa kujitegemea Ernest Munis (pichani juu).
Ndugu Munis ni msharika wa Magomeni na kiongozi wa Fellowship wa Usharika wa Magomeni na pia ni kiongozi wa Fellowship wa jimbo la Kaskazini

Neno kuu lilitoka Mathayo: 12: 1 – 8

Neno la Waraka: Yakobo: 2:8-13

Akihubiri katika ibada hiyo Mwinjilisti Munis alisema Ukristo sio kifungo/utumwa Fulani, bali ni uhuru ndani ya Kristo

Huru maana yake ni kutokua mtumwa wa kitu au kifungo chochote

Kuzaliwa kwa Yesu; kufa kwake na hata kufufuka kwake kulikua ni kumfanya Mristo aweze kuwa huru.Huru katika biashara;kilimo;alie mfanyakazi awe huru;taifa liwe huru; huru katika kila kitu alisema bwana Munis

Mungu hatamani mkristo awe mtumwa wa jambo lolote lile,na hili Mungu alilianza kwenye taifa la Israel kwa kuwatoa katika Utumwa wa Misri

Uhuru wa Yesu unafungua ndoa zilizofungwa, magonjwa yaliyoko ndani yako n.k

Mungu anawatazama Wakristo katika viwango vya tofauti kabisa na walivyo waxhawi au wanga

Mungu mar azote anatuwazia mambo yaliyo mema tu wakati wowote

Mathayo 12:1-8

MAMBO YANAYOWEZA KUMFUNGA MKRISTO;

1.Mashamba /Mazingira

2.Maombi – omba kwa bidii na ukiomba utapewa

3.Imani

Tukiweza kujinasua katika maeneo hayo tutatembea tukiwa huru na hakuna kuwa tena kwenye mateo au kifungo chochote alimalizia mahubiri yake bwana Munis






 Waumini wakiimba kwa hisia nyimbo za kusifu na kuabudu kwenye ibada hiyo ya jumapili


 Waumini mbalimbali pichani juu na chini wakiabudu kwenye ibada hiyo ya jumapili


 Picha juu na chini ni waimbaji wa Kwaya ya Uinjilisti wakihudumu kwenye ibada hiyo ya jumapili katika Usharika wa Mwenge



Ibada hizo zilifanyika mbili, moja ilianza saa moja kamili na ya pili ilianza saa nne kamili asubuhi

No comments:

Leave a Reply