Latest News


More

MAHAFALI ST.DON BOSCO YAFANA DAR ES SALAAM

Posted by : Unknown on : Sunday, December 8, 2013 0 comments
Unknown
Saved under :
MAHAFALI ST.DON BOSCO YAFANA DAR ES SALAAM
Mahafali ya 18 ya shule ya awali ya ST.Don Bosco yamefanyika jana jumamosi na kufana sana.Mahafali hayo yalifanyika katika viwanja vya shule hiyo maeneo ya Sinza karibu na kanisa la Full Gospel Bible Fellowship
Katika mahafali hayo takriban watoto 36 walihitimu ambao mwakani wataingia shule ya msingi
Mgeni rasmi katika mahafali hayo alikua Bwana Arnold ambaye ni mwenyekiti wa kanisa la Roman Catholic parokia ya Sinza

Akimkaribisha mgeni rasmi, mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo bwana David Mfanga alisema shule hiyo inapata mafanikio kila mwaka kwani wanafunzi wanaongezeka kila mwaka ambapo  kwa sasa hivi shule ina uwezo wa kuchukua wanafunzi  120 kwa wakati mmoja

Awali mwaliku mkuu wa shule hiyo alisema shule hii ilianza rasmi mwaka 1995 Januari ikiwa na wanafunzi 40 tu .Hivi sasa shule ina uwezo wa kuchukua wanazunzi 120 kwa wakati mmoja alisema mwalimu huyo.Mikakaiti iliyopo sasa ni kujenga shule ya msingi ambapo kiwanja kimepatikana maeneo ya Mvuti na tayari  mchoro wa ramani ya shule hiyo uko tayari

Shule ya Don Bosco inafundisha masomo yafuatayo;
English, Hesabu, Kiswahili, Sanaa, Afya, Dini na Maadili.Masomo yote yanafundishwa kwa kiingereza isipokuwa Dini na Kiswahili

Shule hii inapokea wanafunzi wa umri wa miaka 2 na nusu mpaka miaka 5 alisema mkuu huyo wa shule.
Changamoto walizo nazo kwa sasa hivi ni kupata fedha za kuchimba kisima cha maji shuleni hapo
Katika mchango wa papo kwa papo uliochangwa ukiongozwa na mgeni rasmi aliyetoa ahadi ya shilingi 500,000 wazazi na walezi walichangia na kupata zaidi ya shilingi milioni moja na laki tatu ambazo ni taslimu na ahadi




No comments:

Leave a Reply