Akizungumza mjini Bethlehem ,papa Francis ametaka kubuniwa kwa taifa huru la Palestina pamoja na Israel.
Aidha alifanya maombi katika eneo ambalo Yesu anadaiwa kuzaliwa.
Akiwa katika ziara yake ya mji wa Bethlehem ,kiongozi huyo wa dini alisimama katika eneo ambalo Israel inajenga ukuta mkubwa pamoja na eneo la West bank ili kufanya maombi.
Maandishi yaliokuwa juu yake alipokuwa akiomba yalisema 'papa tunamtaka mtu atakayezungumzia kuhusu haki'.
No comments: