Latest News


More

MAMBO YA KUZINGATIA KWA KIJANA ANAYETAKA KUFUNGA NDOA

Posted by : Unknown on : Tuesday, April 21, 2015 0 comments
Unknown
Saved under : ,




Ili uweze kujibu swali hilo, unahitaji kujielewa vizuri. Kwa mfano, fikiria mambo yafuatayo:

Mahusiano

Wewe huwatendeaje wazazi wako na ndugu na dada zako? Je, mara nyingi wewe hushindwa kujizuia unapokuwa nao, labda hata kuzungumza kwa ukali au kwa kejeli? Wao wangejibuje ikiwa wangeulizwa swali hilo kukuhusu? Jinsi unavyoshughulika na watu wa familia yako huonyesha jinsi utakavyomtendea mwenzi wako.Waefeso 4:31.

Mtazamo

Je, wewe huwa na mtazamo mzuri au mbaya kuelekea mambo? Je, wewe hukubali maoni ya wengine, au nyakati zote wewe husisitiza mambo yafanywe kwa njia fulani—njia ile wewe unataka? Je, unaweza kuendelea kuwa mtulivu unapokabili hali ngumu? Je, wewe ni mwenye subira? Kusitawisha sifa za tunda la roho ya Mungu sasa kutakusaidia kujitayarisha kwa ajili ya kuwa mume au mke wakati ujao.Wagalatia 5:22, 23.

Gharama

Wewe hushughulikia pesa kwa njia gani? Je, mara nyingi wewe hujikuta ukiwa na madeni? Je, unaweza kudumisha kazi? Ikiwa huwezi, sababu ni nini? Je, tatizo ni kazi yenyewe? Je, tatizo ni mwajiri? Au je, ni kwa sababu ya zoea au tabia fulani unayohitaji kufanyia kazi? Ikiwa ni vigumu kwako kushughulikia gharama zako mwenyewe, utashughulikiaje za familia yako?1 Timotheo 5:8.

Hali ya Kiroho

Ikiwa wewe ni Shahidi wa Yehova, una sifa gani za kiroho? Je, wewe husoma Neno la Mungu, kushiriki katika huduma, na kutoa maelezo katika mikutano ya Kikristo? Yule utakayefunga ndoa naye anastahili kuwa na mwenzi mwenye nguvu kiroho.Mhubiri 4:9, 10.

Kadiri unavyojielewa, ndivyo utakavyoweza kumpata mtu atakayekusaidia kukuza sifa zako nzuri badala ya udhaifu wako

No comments:

Leave a Reply