Written by Anonymous

HAPPY NEW YEAR 2015

by Anonymous / 06 Jan 2015

...

Written by Anonymous

MERY CHRISTMAS

by Anonymous / 25 Dec 2014

WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRIS...

Written by Anonymous

HAMUGEMBE PRAISE AND WORSHIP TEAM KUZINDUA ALBUM YAO MWEZI APRIL

by Anonymous / 31 Mar 2014

 Kikundi cha Hamugembe Praise and Worship Team cha mjini Bukoba  kinatarajia kuzindua album yao ya nyimbo za kusifu na kuabudu ...

Written by Anonymous

WE WISH YOU A HAPPY NEW YEAR 2014

by Anonymous / 31 Dec 2013

Leo ndio siku ya mwisho kwa mwaka huu 2013 na masaa machache yajayo tutaingia mwaka ujao 2014.Mtandao huu unawatakia kila la kheri na ba...

Written by Anonymous

KWAYA KUU YA USHARIKA WA AZANIA FRONT NDIO MABINGWA WA UIMBAJI WA K.K.K.T – DMP

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

Written by Anonymous

MASHINDANO YA UIMBAJI KWAYA KUU NGAZI YA DAYOSISI YA KANISA LA K.K.K.T (DMP) YAFANA USHARIKA WA MBEZI BEACH LEO

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

KUTOKA MADHABAHUNI

IBADA KATIKA KANISA LA LIVING WATER CENTER MAKUTI KAWE JUMAPILI HII

Jumapili hii ilifanyoka ibada nzuri katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe ambapo kiongozi wa kanisa hilo Mtume Onesmo Ndegi  (pichani juu) aliongoza na kuhubiri Pichani juu Mtume Onesmo Ndegi akimtambulisha ndugu wa m...

More KUTOKA MADHABAHUNI
More NENO LA LEO
More MAHUBIRI
More MAOMBI

HABARI ZA KIDINI

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MHESHIMIWA MAKONDA AZINDUA VITABU VYA INJILI KANISA LA LIVING WATER CENTER KAWE KAWE

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mheshimiwa Paul Makonda jumapili hii alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa vitabu vya injili vya mwalimu Lilian Ndegi katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe Bwana Makonda (pichani juu) alimsh...

More HABARI ZA KIDINI

More HABARI ZA KIDINI

Fedha zisizo halali hatari kwa familia

Posted by : Unknown on : Thursday, July 25, 2013 0 comments
Unknown
Saved under :
WAAMINI wa Kanisa Katoliki nchini wametakiwa kuacha tabia ya kutafuta fedha kwa njia zisizo halali na kuzipeleka nyumbani kwa matumizi ya familia kwa sababu fedha hizo hazitakuwa na baraka kwa watoto wao.
Paroko Msaidizi wa Parokia ya Kurasini, Padri Marcel Mukadi alisema suala la kutafuta fedha kwa njia zisizo halali ikiwemo kuwa na ndimi mbili ni kuharibu maisha yao.
Akitoa Mahubiri wakati wa ibada ya misa takatifu kwa Wanahija wa Kanda  ya Mtakatifu  Martin de Pores iliyopo katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Maurus Kurasini waliofanya hija katika Kituo cha Mbagala Msalabani, Padri Mukadi alisema:
“Angalieni maisha ya undumilakuwili si mazuri utapenda kumfurahisha mmoja zaidi ya mwingine na kuwa nafsi yao itakuwa ikifadhaika kwa kufanya vitendo hivyo na kamwe hautakuwa na furaha kuwa na majukumu mawili mawili kwa wakati mmoja kunaharibu maisha maana ndimi mbili hazikai pamoja”.
Aliendelea kusema wanahija hao waache kuwa vitendo vya ndimi mbili kwa kuwa vinasababisha waamini washindwe kumuabudu Mungu kwa wakati na kwa njia iliyo nyoofu kutokana na kushika mambo mawili ambayo ni ya Mungu na ya Shetani.
Alisema waamini wamekuwa wakishiriki katika vitendo vya ushirikina kutafuta fedha ili kuwa na maisha mazuri kitu ambacho ni hatari kwa sababu fedha watakazozipata zitakuwa ni za majuto hapo baadaye mara maisha yao yatakapoharibika.

Padri Marcel alisema fedha wanazozipata kwa njia hiyo ya ushirikina huziharibu familia zao hasa watoto ambao baadaye wanaweza kupata madhara bila ya wao kujua.
Paroko huyo alitoa onyo kwa Waamini hao kuacha tabia ya kupeleka fedha nyumbani kwa matumizi ya familia zilizopatikana kwa njia isiyokuwa halali ili kuwanusuru watoto wasio na hatia.
“Unaenda kwa waganga wa kienyeji unapata fedha na kuzirudisha nyumbani unafikiri mwisho wake ni nini ni kuwa watoto mazezeta halafu unalalamika hebu fikiria wewe unakula rushwa kwa ajili ya kitu fulani kizuri unafikiri rushwa itajenga maisha yako kama umechukua rushwa basi tumia wewe mwenyewe na si kuipeleka nyumbani kwa Watoto”,alisema Padri Marcel.
Hata hivyo alifahamisha kwamba vitendo vya utoaji mimba navyo ni hatari kwa maisha yao kwa sababu vitakuwa mwiba punde watakapozaa watoto wengine kutokana na watoto waliowapotezea maisha kwa kutoa mimba kuwalilia.
Padri Marcel alisema watoto watakaozaliwa na mtu aliyetoa mimba hawatakuwa na maisha mazuri hivyo Yesu waliyemfuata katika kituo hicho cha hija Mbagala awe kidole cha kuwaonesha mguu wao ukae wapi kwa kutawala maisha katika maisha yao yao huku Roho Mtakatifu akiwa Kiongozi wao kwa kuwa alisema ‘waonje ya kuwa bwana ni mwema.

Akitoa mfano wa Mtakatifu Paulo alivyomlilia Mungu kutokana na majivuno yake Padri Marcel alisema mtume huyo alikuwa na afya iliyozorota hana uwezo wa  kuhubiri Injili licha kuwa na elimu ya dini kutokana na udhaifu huo alimlilia Mungu ili awe na uwezo huo wa kuhubiri lakini Mungu alimwambia neema yake inatosha hivyo aliwataka waamini hao kumlilia Mungu ili aweze kuwapatia neema katika maisha yao.
Alisema wapo wahubiri katika Agano la kale waliojaliwa uwezo wa kuhubiri habari njema waliokuwa wakimcheka Mtume Paulo kwa afya aliyokuwa nayo kwa sababu Mungu alimpa uwezo.
“Paulo alikuwa na afya iliyozorota alikuwa Mfarisayo na alikuwa na elimu ya dini lakini hakuwa na kipaji katika kuhubiri hivyo alisema nilimuomba Mungu kwa ajili ya majivuno yangu nisije nikajivuna kupita kiasi naye akaniambia neema yangu yatosha hivyo tujifunze kutokana na Paulo alivyowekewa mwiba mwilini mwake asije kuwa na majivuno”.

“Tujifunze kuwa Mungu ana uwezo wa kufanya chochote ndani yetu anaweza kukupa gari na akaliharibu kwa ajali hivyo leo Mungu anasema neema yake inatutosha ni kwamba hakuna kitu kinachotendeka ndani yetu bila ya sababu bali tuseme neema yake yatutosha tunapokuwa katika majaribu yake tumrudie yeye ndiye kila kitu katika maisha yetu”,alisema Padri Marcel.
Kabla ya Ibada hiyo ya misa takatifu, Padri Marcel alitoa semina kwa wanahija hao kuhusu Mama Bikira Maria na kueleza kwamba hija ni safari ya kwenda kumuomba Mungu na kupata neema ambayo kila mtu aliyekwenda kuhiji anakuwa na lengo lake binafsi la kuomba.
Padri Marcel aliwataka Wanahija hao kuangalia msalaba huo na kuona uwepo wa Mama Bikira Maria chini yake kama maandiko yanavyosema wakati Yesu Kristo alipokuwa msalabani kwa kumwambia Yohane mtoto tazama Mama yako na Mwanamke tazama mwanao hivyo wamchukue Bikira Maria na kwenda naye nyumbani mwao.
Alibainisha kama ilivyokuwa maana ya hija ni safari lakini umbali wa wao kufika katika kituo hicho cha hija ni mfupi hivyo lengo lao ni kuwa na Yesu ndiyo maana wamefika hapo chini ya Msalaba hivyo kama wataomba kwa imani kupitia mama Bikira Maria aliye chini ya Msalaba huo watafanikiwa.
Alidokeza Mama Bikira Maria alikuja duniani ili kuleta uhai baada ya mwanadamu kuleta kifo ndiyo maana Mungu alimuandaa ili amzae Emanuel na hivyo kuweka agano jipya kwake na kuwataka Waamini hao kumpelekea shida zao ili aweze kuwasaidia kwa kuzipeleka kwa mwanae Yesu Kristo kama alivyofanya katika harusi ya Kana walivyoishiwa divai.
Kituo cha Hija cha Mbagala kilianza kufahamika kwenye Jubilei kuu ya miaka 2000 baada ya kuzaliwa Kristo na kuteuliwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam Polycarp Kardinali Pengo kuwa ni kituo cha hija kutokana na Msalaba uliosimikwa na Padri Maurus Hartmann kabla ya vita ya kwanza  ya Dunia mwaka 1914-1918 ulioonesha ni eneo la kuwazika wakristo.

Baada ya kutangazwa kuwa ni kituo cha hija Wanaparokia wa Kituo cha Kiroho cha  Mbagala hasa waliokuwa wakiishi karibu na Kituo hicho walihamasika na kuanza kusafisha eneo hilo la Msalaba na kulizungushia ukuta ambapo baada ya Jubilei kuu watu wamekuwa wakienda kusali.
Msalaba huo ulitokana na umuhimu wa kuwepo kwa mahali pa kuzikia watu baada ya Padri Maurus kununua eneo hilo la Mbagala mwaka 1901 baada ya Kurasini,eneo la Kurasini kuonekana halifai kwa kilimo na hivyo kuwahamishia Vijana hao waliokuwa wakitunzwa na Kanisa la Kurasini baada ya kukombolewa kwenye biashara ya utumwa.
Aidha hata wale waliokuwa yatima walitunzwa katika eneo hilo la Mbagala ambapo makaburi hayo yalikuwepo hadi mwaka 1971 na kuharibiwa na watu waliokuwa wakitafuta viwanja

No comments:

Leave a Reply