Latest News


More

Papa Francis azuru eneo hatari Brazil

Posted by : Unknown on : Saturday, July 27, 2013 0 comments
Unknown
Saved under :


Rio de Janeiro, Brazil
Papa Francis amezuru eneo hatari lenye uhalifu mwingi mjini humu na kusema vijana ndio chachu ya mabadiliko na maendeleo ya imani katika Kanisa Katoliki duniani.
Katika ziara yake kwenye makazi ya watu maskini na uhalifu mwingi uliokithiri ya Varginha, Papa Francis alisema kuwa vijana hawana budi kuingia mitaani kuhubiri Injili bila hofu, woga na kueleza kuwa kanisa lisilowafikia wengi hugeuka chama cha kiraia au cha kibinadamu.
“Mkifanya hivyo, sina shaka majimbo yenu yatabadilika pia, imani itakuwa na mizizi na neno la Mungu litawafikia wengi.
“Msifanye mzaha, fanyeni fujo katika kuhubiri,” alisema Papa Francis katika hotuba kwenye ufunguzi wa Siku ya Vijana Duniani kwenye ufukwe maarufu wa Copacabana uliojaa maji, matope kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
“Ninataka kuona fujo majimboni mwenu!” alisema kwa Kispaniola na kuongeza: “Ninataka kuona kanisa likiwa karibu na watu.
“Ninataka kuona mnaachana na mazoea kwamba uinjilishaji ni kazi ya makasisi, kanisa la kujifungia ndani ya parokia zenu, shule au zahanati zenu. Ninataka mtoke nje!”
Saved under :

No comments:

Leave a Reply