Homa ya ini ni ugonjwa
hatari kuliko Ukimwi
Ugonjwa
wa selimundu unasumbua wengi, umetengua ndoa za wengine, kwa sababu ya kutojua.
Hakuna
shaka kwamba umewahi kusafiri nje ya nchi yako na kutakiwa kupata chanjo.
Kwa
wengine, chanjo hiyo ikiwamo ya homa ya ini imeonekana kama usumbufu na
udhia mtupu. Hata hivyo, wapo wengine ambao hawaufahamu ugonjwa huu.
Kwa
wanaoujua, wanahofia kuwa ugonjwa huu una madhara makubwa pengine kuliko
saratani na Ukimwi.
Homa hiyo
au Hepatitis B inapewa uzito mdogo licha ya kuwa ni ya hatari kubwa.
Wataalamu
wanaeleza kuwa Hepatitis B au homa ya ini ni ugonjwa unaoambukizwa kwa urahisi,
wenye madhara makubwa na wenye uwezo wa kuambukiza kwa wepesi kuliko Ukimwi.
Kitaalamu,
ugonjwa huu, husababishwa na virusi vya Hepatitis B (HBV) ambavyo
huathiri mfumo wa utoaji wa sumu mwilini. Inaelezwa kuwa robo tatu ya
watu ulimwenguni wameathiriwa kwa muda na homa ya ini na wengine milioni 350
wameathirika moja kwa moja.
No comments: