Latest News


More

Je wajua kuwa Homa ya ini ni ugonjwa hatari kuliko Ukimwi?

Posted by : Unknown on : Sunday, August 25, 2013 0 comments
Unknown
Saved under :


Homa ya ini ni ugonjwa hatari kuliko Ukimwi

Ugonjwa wa selimundu unasumbua wengi, umetengua ndoa za wengine, kwa sababu ya kutojua.
Hakuna shaka kwamba umewahi kusafiri nje ya nchi yako na kutakiwa kupata chanjo.
Kwa wengine, chanjo hiyo ikiwamo ya homa ya ini imeonekana kama usumbufu na  udhia mtupu. Hata hivyo, wapo wengine ambao hawaufahamu ugonjwa huu.
Kwa wanaoujua, wanahofia kuwa ugonjwa huu una madhara makubwa pengine kuliko  saratani na Ukimwi.

Homa hiyo au Hepatitis B inapewa uzito mdogo licha ya kuwa ni  ya hatari kubwa.
Wataalamu wanaeleza kuwa Hepatitis B au homa ya ini ni ugonjwa unaoambukizwa kwa urahisi, wenye madhara makubwa na wenye uwezo wa kuambukiza kwa wepesi kuliko Ukimwi.
Kitaalamu, ugonjwa huu, husababishwa na virusi vya Hepatitis B (HBV) ambavyo huathiri  mfumo wa utoaji wa sumu mwilini. Inaelezwa kuwa robo tatu ya watu ulimwenguni wameathiriwa kwa muda na homa ya ini na wengine milioni 350 wameathirika moja kwa moja.

No comments:

Leave a Reply