Texas – Marekani
Mchungaji wa kanisa la Resurrecting Faith la mjini Texas
Marekani amepiga marufuku waumini wake kuvaa nywele bandia maarufu kama wigi na kuwataka wahakikishe wanakwenda na nywele
zao za asili katika ibada za kanisa hilo
Katika agizo hilo alilolitoa wiki hii, mchungaji huyo
aliwataka kuhudhuria ibadani kama walivyo bila kubadili nywele zao au kutumia dawa au kuvaa nywele bandia
Marekani yenye mchanganyiko wa watu kutoka maeneo mengi
duniani imekuwa na tamaduni tofauti
ambapo watu weusi hasa wenye asili ya Afrika wamekuwa wakijaribu kuvaa mavazi
tofauti na kubadili nywele zao za asili
Katika mahojiano maalum na tovuti moja ya masuala ya kidini
nchini Marekani mchungaji huyo aliyetambuliwa kwa jina la Amir anayeongoza
kanisa la Resurrecting Faith huko Waco, Texas aliwaeleza waumini wake kwamba
nywele bandia zinawasilisha dhana ya wanawake kutojiamini , kutojitambua na
kutojikubali
No comments: