Hukumu ya mwisho iko na kial mtu atahukumiwa kulingana na makosa na maisha aliyoyaishi kwenye dunia hii
Akihubiri kwenye ibada ya jumapili hii Mchungaji Tumsifu Kweka (pichani juu) alisema maisha tunayoishi sasa hivi ndiyo kielelezo cha maisha yetu yajayo
Akisoma neno toka Kumb.6:6 - 7 alisema ni budi wakristo kuishi maisha yanayompendeza na kumtukuza Mungu ili kuepuka hukumu ijayo kwani ipo na hakuna njia nyingine ya kuikwepa zaidi ya kumkubali Yesu Kristo kama bwana na mwokozi wa maisha yetu
Waumini wakifuatilia mahubiri usharikani Mwenge
Mchungaji Kweka akiwa na mwinjilisti Mwigune madhabahuni
Kwaya ya Sekondari ya Alpha ikiimba kwenye ibada hiyo
Mchungaji Kweka ni mchungaji wa Usharika wa Nkuarungo, jimbo la Hai katika Dayosisi ya Kaskazini
Ibada hiyo iliongozwa na mwinjilisti wa Usharika wa Mwenge mwinjilisti Mwigune na mahubiri Mchungaji Kweka
No comments: