Written by Anonymous

HAPPY NEW YEAR 2015

by Anonymous / 06 Jan 2015

...

Written by Anonymous

MERY CHRISTMAS

by Anonymous / 25 Dec 2014

WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRIS...

Written by Anonymous

HAMUGEMBE PRAISE AND WORSHIP TEAM KUZINDUA ALBUM YAO MWEZI APRIL

by Anonymous / 31 Mar 2014

 Kikundi cha Hamugembe Praise and Worship Team cha mjini Bukoba  kinatarajia kuzindua album yao ya nyimbo za kusifu na kuabudu ...

Written by Anonymous

WE WISH YOU A HAPPY NEW YEAR 2014

by Anonymous / 31 Dec 2013

Leo ndio siku ya mwisho kwa mwaka huu 2013 na masaa machache yajayo tutaingia mwaka ujao 2014.Mtandao huu unawatakia kila la kheri na ba...

Written by Anonymous

KWAYA KUU YA USHARIKA WA AZANIA FRONT NDIO MABINGWA WA UIMBAJI WA K.K.K.T – DMP

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

Written by Anonymous

MASHINDANO YA UIMBAJI KWAYA KUU NGAZI YA DAYOSISI YA KANISA LA K.K.K.T (DMP) YAFANA USHARIKA WA MBEZI BEACH LEO

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

KUTOKA MADHABAHUNI

IBADA KATIKA KANISA LA LIVING WATER CENTER MAKUTI KAWE JUMAPILI HII

Jumapili hii ilifanyoka ibada nzuri katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe ambapo kiongozi wa kanisa hilo Mtume Onesmo Ndegi  (pichani juu) aliongoza na kuhubiri Pichani juu Mtume Onesmo Ndegi akimtambulisha ndugu wa m...

More KUTOKA MADHABAHUNI
More NENO LA LEO
More MAHUBIRI
More MAOMBI

HABARI ZA KIDINI

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MHESHIMIWA MAKONDA AZINDUA VITABU VYA INJILI KANISA LA LIVING WATER CENTER KAWE KAWE

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mheshimiwa Paul Makonda jumapili hii alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa vitabu vya injili vya mwalimu Lilian Ndegi katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe Bwana Makonda (pichani juu) alimsh...

More HABARI ZA KIDINI

More HABARI ZA KIDINI

KANISA HUKO DODOMA LAFUNGA KUOMBEA BUNGE LA KATIBA

Posted by : Unknown on : Saturday, March 29, 2014 0 comments
Unknown
“Kwa hali ilivyo sasa bungeni, tusitegemee kupata Katiba au ikipatikana inaweza kutokidhi matakwa ya wananchi kwa sababu tayari wanaoitengeneza wamegawanywa. Tunamwomba Mungu aingilie kati.” Lucas Mwakalonge 
Dodoma. Kanisa la Makole Pentekoste Holyness la mjini hapa, linafanya maombi maalumu ya kuliombea Bunge Maalumu la Katiba baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa Bunge hilo.
Maombi hayo yaliyoanza Jumatatu, yanatarajiwa kumalizika Jumapili ijayo kwa waumini kugawanyika makundi, kila moja linaomba kwa kufunga kwa siku moja kabla ya kujumuika pamoja kanisani, Jumapili kuomba kwa pamoja.
“Kificho (aliyekuwa mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo) aliliongoza bila kanuni ingawa kulikuwa na mvutano haukuwa mkubwa na alipochaguliwa Sitta kuwa mwenyekiti wa kudumu wananchi wengi tulifurahi,” Mchungaji Kiongozi Asajile Mwandiga alisema na kuongeza.
“Kwa tulivyomfahamu uwezo wake wa kuongoza, kwa mfano Bunge la Tanzania la 9, tuliamini tungepata Katiba bora lakini imekuwa kinyume, anaegemea upande wa chama chake kwa uwazi kabisa.”
Mch. Mwandiga alisema hali hiyo iliwakatisha tamaa, lakini kwa kuwa wanaamini katika Mungu, sasa wanaongoza Kanisa kuomba msaada wake ili abadilishe mioyo ya wanaopindisha mambo.
Naye Mchungaji kiongozi msaidizi wa kanisa hilo, Lucas Mwakalonge, alisema tofauti na Bunge kuamua mambo kwa mtindo wa wengi wape, wao wanaoamini katika Mungu.
Mwakalonge alitaja sababu nyingine za maombi hayo kuwa ni mivutano ya mara kwa mara bungeni kiasi cha vikao kuvunjika na mgawanyiko wa Wabunge wa Bunge Maalumu.
Mchungaji huyo aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maktaba na Tafiti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano hadi alipostaafu mwaka 2011, alisema ili kufikia uamuzi wa kutoa Katiba bora ni lazima kuwe na umoja miongoni mwa wanaoiunda na kuiandika.
“Kwa hali ilivyo sasa bungeni, tusitegemee kupata Katiba au ikipatikana inaweza kutokidhi matakwa ya wananchi kwa sababu tayari wanaoitengeneza wamegawanywa. Tunamuomba Mungu aingilie kati,” alieleza.
Mbali na hayo, Mwakalonge alisema wanataka uwezo wa Mungu uzuie mambo yasiyompendeza kuingizwa kwenye Katiba, akitoa mfano wa sura ya 4 inayohusu Haki za Binadamu, kwamba kusiwe na utetezi wa mashoga na wasagaji.
“Kuna mambo hakika hayapaswi kuingizwa kwenye katiba yetu, tunamuomba Mungu apitishie mbali wale wote wanaotaka kuifanya katiba hii kama mchezo wa kuigiza,” alisema
(Chanzo:Mwananchi Communication)

No comments:

Leave a Reply