Written by Anonymous

HAPPY NEW YEAR 2015

by Anonymous / 06 Jan 2015

...

Written by Anonymous

MERY CHRISTMAS

by Anonymous / 25 Dec 2014

WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRIS...

Written by Anonymous

HAMUGEMBE PRAISE AND WORSHIP TEAM KUZINDUA ALBUM YAO MWEZI APRIL

by Anonymous / 31 Mar 2014

 Kikundi cha Hamugembe Praise and Worship Team cha mjini Bukoba  kinatarajia kuzindua album yao ya nyimbo za kusifu na kuabudu ...

Written by Anonymous

WE WISH YOU A HAPPY NEW YEAR 2014

by Anonymous / 31 Dec 2013

Leo ndio siku ya mwisho kwa mwaka huu 2013 na masaa machache yajayo tutaingia mwaka ujao 2014.Mtandao huu unawatakia kila la kheri na ba...

Written by Anonymous

KWAYA KUU YA USHARIKA WA AZANIA FRONT NDIO MABINGWA WA UIMBAJI WA K.K.K.T – DMP

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

Written by Anonymous

MASHINDANO YA UIMBAJI KWAYA KUU NGAZI YA DAYOSISI YA KANISA LA K.K.K.T (DMP) YAFANA USHARIKA WA MBEZI BEACH LEO

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

KUTOKA MADHABAHUNI

IBADA KATIKA KANISA LA LIVING WATER CENTER MAKUTI KAWE JUMAPILI HII

Jumapili hii ilifanyoka ibada nzuri katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe ambapo kiongozi wa kanisa hilo Mtume Onesmo Ndegi  (pichani juu) aliongoza na kuhubiri Pichani juu Mtume Onesmo Ndegi akimtambulisha ndugu wa m...

More KUTOKA MADHABAHUNI
More NENO LA LEO
More MAHUBIRI
More MAOMBI

HABARI ZA KIDINI

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MHESHIMIWA MAKONDA AZINDUA VITABU VYA INJILI KANISA LA LIVING WATER CENTER KAWE KAWE

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mheshimiwa Paul Makonda jumapili hii alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa vitabu vya injili vya mwalimu Lilian Ndegi katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe Bwana Makonda (pichani juu) alimsh...

More HABARI ZA KIDINI

More HABARI ZA KIDINI

TUNAWEZAJE KUMKUMBUKA BWANA YESU KRISTO?

Posted by : Unknown on : Thursday, May 21, 2015 0 comments
Unknown
Saved under :

Yesu Kristo—Tumkumbuke kwa Njia Gani?

Mwezi wa Desemba watu wengi ulimwenguni pote huona picha za Yesu akiwa mtoto. Akiwa amelazwa kwenye hori, yaani, sanduku kubwa linalotumiwa kulishia wanyama. Lakini je, tunapaswa kumkumbuka Yesu akiwa mtoto tu? * Acheni tuzungumzie njia muhimu zaidi ya kumkumbuka. Tunaweza kujifunza kutokana na jambo lililowapata wachungaji waliokuwa malishoni karibu na Bethlehemu usiku mmoja.
Ghafula malaika anawatokea wachungaji hao. Anawaambia hivi: “Mwokozi ambaye ni Kristo Bwana, amezaliwa kwenu.” Pia, malaika anawaambia watampata Yesu “akiwa amefungwa vitambaa na akiwa amelala katika hori.” Papo hapo, malaika wengine wengi wanatokea na kuanza ‘kumsifu Mungu.’
Ungehisije kama ungewasikia malaika wakimsifu Mungu?— Wachungaji wanafurahi sana! Wanasema: “Na twende moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukaone jambo hili ambalo limetendeka.” Wanapofika huko wanamkuta “Maria na vilevile Yosefu, na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori.”
Baadaye watu wengine wanakuja Bethlehemu ambako Maria na Yosefu wanakaa. Wachungaji wanapowaambia kuhusu kilichotukia, wote wanashangaa. Je, unafurahi kujua mambo hayo yenye kustaajabisha?— Watu wanaompenda Mungu wanafurahi kuyajua. Sasa acheni tuone ni kwa nini watu wanafurahi sana baada ya Yesu kuzaliwa. Ili tuelewe jambo hilo, tutachunguza mambo yaliyotukia kabla Maria hajaolewa.
Siku moja malaika anayeitwa Gabrieli anamtembelea Maria. Anamwahidi kwamba atazaa mtoto ambaye “atakuwa mkuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi.” Pia, Gabrieli anasema: “Atatawala akiwa  mfalme . . . na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”
Maria anataka kujua hilo litawezekanaje kwa kuwa hajawahi kulala na mwanamume. Basi, Gabrieli anamfafanulia: “Nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika,” na “kile kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.” Huo ungekuwa muujiza mkubwa! Kuuhamisha uhai wa Mwana wa Mungu kutoka mbinguni na kuuweka ndani ya tumbo la uzazi la Maria.
Je, umewahi kuona picha zinazoonyesha wanaume watatu wenye hekima pamoja na wachungaji wakimtembelea mtoto Yesu?— Ni jambo la kawaida kuona picha hizo wakati wa Krismasi. Lakini hazionyeshi jambo sahihi. Wanaume hao watatu walikuwa wanajimu, walizoea kufanya jambo ambalo Mungu alikataza. Acheni tuone kilichotukia walipofika. Biblia inasema: “Walipoingia ndani ya ile nyumbawakamwona huyo mtoto mchanga pamoja na Maria mama yake.” Wakati huo Yesu hakuwa mtoto aliyetoka tu kuzaliwa ndani ya hori; bali alikuwa akiishi pamoja na Yosefu na Maria katika nyumba!
Wanajimu walimpataje Yesu?— Ile “nyota” haikuwaongoza kwenda Bethlehemu kwanza, bali iliwaelekeza kwa Mfalme Herode huko Yerusalemu. Biblia inasema Herode alitaka kumpata Yesu ili amuue. Sasa fikiria jambo hili. Unafikiri ni nani aliyetumia kitu kilichofanana na nyota kuwaongoza wale wanajimu kwa Herode?— Si Yehova, Mungu wa kweli, bali ni mpinzani na adui yake, Shetani Ibilisi!
Leo, Shetani anawafanya watu wamfikirie Yesu kuwa mtoto aliyetoka tu kuzaliwa. Lakini Malaika Gabrieli alimwambia hivi Maria: “[Yesu] atatawala akiwa mfalme . . . , na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” Sasa anatawala akiwa Mfalme huko mbinguni, na hivi karibuni atawaangamiza adui wote wa Mungu. Hilo ndilo jambo tunalopaswa kukumbuka kumhusu Yesu, na tunapaswa kuwaambia wengine kulihusu.
(Source:www.jw.org)

No comments:

Leave a Reply