Latest News


More

UNAWEZAJE KUWAWALEA WATOTO KATIKA ULIMWENGU WENYE UBINAFSI

Posted by : Unknown on : Thursday, March 26, 2015 0 comments
Unknown
Saved under :

Kulea Watoto Wenye Kujali Katika Ulimwengu Wenye Ubinafsi


KILA siku watu hupata fursa nyingi za kuwatendea wengine kwa fadhili. Hata hivyo, inaonekana kwamba watu wengi hujifikiria tu. Unaweza kuona jambo hilo kila mahali—jinsi watu wanavyowapunja wengine bila aibu, jinsi wanavyoendesha magari bila kujali, jinsi wanavyotumia lugha chafu na wanavyolipuka kwa hasira.
Mtazamo wa “mimi kwanza” pia unaonekana katika familia nyingi. Kwa mfano, wenzi fulani hutalikiana kwa sababu tu mwenzi mmoja anahisi anastahili kuwa na mtu bora kuliko yule aliye naye sasa. Bila kujua, wazazi wengine pia wanaweza kukuza mtazamo wa ubinafsi katika watoto wao. Jinsi gani? Kwa kumpa mtoto chochote anachotaka, na kusita kumpa nidhamu yoyote.
Tofauti na hilo, wazazi wengi wanawazoeza watoto wao kutanguliza masilahi ya wengine, na wanapata faida kubwa. Watoto wanaowajali wengine wanaweza kuanzisha na kufurahia urafiki wenye kudumu. Pia wanaweza kuwa na uradhi. Kwa nini? Kwa sababu kama Biblia inavyosema, “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.
Ikiwa wewe ni mzazi, unawezaje kuwasaidia watoto wako wapate faida za kuwa wenye fadhili na waepuke kuathiriwa na mtazamo wa kujifikiria ambao umeenea? Chunguza mambo matatu yanayoweza kumfanya mtoto wako awe na mtazamo wa “mimi kwanza,” na jinsi ambavyo unaweza kuyaepuka.

 1 Kumsifu Mtoto Kupita Kiasi

Tatizo. Watafiti wameona mwelekeo usiofaa: Vijana wengi wanapoanza kufanya kazi wanakuwa na mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu—mtazamo huo unawafanya wadai mafanikio hata ikiwa hawajafanya chochote kustahili mafanikio hayo. Baadhi yao hudhani kwamba watapandishwa cheo haraka, hata kabla ya kuwa stadi katika kazi yao. Wengine wanajiona kuwa bora na kwamba wanastahili kutendewa hivyo—wasipotendewa hivyo, wanashuka moyo.
Kisababishi ni nini? Nyakati nyingine huenda mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu ukatokana na malezi ya mtu. Kwa mfano, wazazi fulani wameathiriwa sana na wazo ambalo limeendelezwa katika miaka ya karibuni kwamba kujiheshimu ndilo jambo muhimu zaidi na linapaswa kuzingatiwa. Ilisemekana kwamba wazo hilo linafaa kwa kuwa ikiwa mtoto anafaidika anaposifiwa kidogo, basi akisifiwa sana atafaidika zaidi. Kwa upande mwingine, ilisemekana kwamba kumwonyesha mtoto kwamba hufurahishwi na mambo anayofanya kutamvunja moyo. Na mzazi aliyefanya hivyo alionwa kuwa mzazi asiyefaa kwani ulimwengu ulikuwa na lengo la kuwafanya watu wajiheshimu. Wazazi waliambiwa kwamba hawapaswi kumfanya mtoto ahisi kuwa amekosea.
Kwa sababu hiyo, wazazi wengi walianza kuwasifu sana watoto wao hata wakati ambapo hawakufanya jambo lolote linalostahili sifa. Mtoto alipotimiza jambo lolote, hata liwe dogo kiasi gani, alisifiwa; alipofanya makosa, hata yawe makubwa kiasi gani, yalipuuzwa. Wazazi waliamini kwamba siri ya kumfanya mtoto ajiheshimu ni kupuuza makosa na kusifu jambo lingine lolote. Kuwafanya watoto wajihisi vizuri kukawa jambo muhimu zaidi kuliko kuwafundisha kujitahidi kutimiza mambo ambayo yatawafanya wajihisi vizuri.
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba mtu anapaswa kusifiwa anapostahili. (Mathayo 25:19-21) Lakini kuwasifu watoto ili tu wajihisi vizuri kunaweza kuwafanya wawe na maoni yasiyofaa kujihusu. Biblia inasema hivi kwa kufaa: “Yeyote akifikiri kuwa yeye ni kitu wakati yeye si kitu, anaidanganya akili yake mwenyewe.” (Wagalatia 6:3) Kuna sababu nzuri kwa nini Biblia inawaambia wazazi: “Usimnyime mvulana nidhamu. Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa.” *Methali 23:13.
Mambo unayoweza kufanya. Fanya iwe lengo lako kumrekebisha mtoto inapohitajiwa na kumsifu anapostahili kikweli. Usiwasifu watoto kwa sababu tu unataka kuwafanya wajihisi vizuri. Huenda hawatafaidika. Kitabu Generation Me kinasema: “Mtu hujiheshimu kikweli kwa sababu ya kuboresha vipawa vyake na kujifunza mambo, hajiheshimu kwa sababu tu ya kusifiwa bila sababu.”
“Msijifikirie kuwa watu wa juu kuliko mlivyo. Badala yake, muwe na kiasi.”—Warumi 12:3, Neno—Agano Jipya

 2 Kumlinda Kupita Kiasi

Tatizo. Imeonekana kwamba vijana wengi huwa hawajajitayarisha kukabiliana na matatizo wanapoanza kufanya kazi. Wengine huvunjika moyo sana wanapochambuliwa kidogo tu. Wengine hawakubali kufanya kazi yoyote isipokuwa ile inayowapendeza. Kwa mfano, katika kitabu Escaping the Endless Adolescence, Dakt. Joseph Allen anasimulia kuhusu kijana mmoja ambaye alimwambia hivi alipokuwa akimhoji kwa ajili ya kazi fulani: “Ninaona kwamba sehemu fulani za kazi hii zinaweza kunichosha, nami sitaki kuchoka.” Dakt. Allen anaandika hivi: “Inaonekana hakuelewa kwamba kazi zote huwa na mambo fulani yanayochosha. Mtu anawezaje kuwa na umri wa miaka 23 na asijue jambo hilo?”
Kisababishi ni nini? Katika miaka ya hivi karibuni, wazazi wengi wameamua kuwalinda watoto wao kutokana na matatizo ya aina yoyote. Kwa sababu hiyo, binti yao anapopata alama za chini katika mtihani, wazazi huingilia kati na kumlazimisha mwalimu ampe alama za juu. Au, mwana wao anapoharibu kitu fulani anapocheza, wazazi huingilia na kumlipia. Au mwana wao anapozozana na rafiki yake, wazazi humlaumu rafiki yake.
Ingawa ni jambo la kawaida kutaka kuwalinda watoto wako, unapowalinda kupita kiasi unaweza kuwafunza jambo lisilofaa—kwamba hawahitaji kuwajibika kwa matendo yao. “Badala ya kujifunza kwamba wanaweza kukabiliana na uchungu na mambo yanayokatisha tamaa, na kujifunza jambo fulani kutokana nayo,” kinasema kitabu Positive Discipline for Teenagers, “watoto [hao] huwa watu wazima ambao ni wenye ubinafsi sana, wakiwa na maoni ya kwamba kila mtu, kutia ndani wazazi wao, wanapaswa kuwatimizia mahitaji yao.”

Biblia inasema nini? Matatizo ni sehemu ya maisha. Kwa kweli Biblia inasema: “Mambo mabaya huwapata watu wote!” (Mhubiri 9:11, Easy-to-Read Version) Hilo linatia ndani watu wazuri. Kwa mfano, Paulo, mtume Mkristo alivumilia matatizo ya aina mbalimbali alipokuwa akihubiri. Hata hivyo, kukabiliana na matatizo hayo kulimletea faida! Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwa mwenye kujitosheleza katika hali zozote nilizo nazo. . . . Nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kupatwa na uhitaji.”—Wafilipi 4:11, 12.
Mambo unayoweza kufanya. Ukizingatia ukomavu wa watoto wako, jitahidi kufuata kanuni hii ya Biblia: “Kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) Mwana wako akiharibu kitu fulani anapocheza, ingefaa umwache alipie kitu hicho. Binti yako akipata alama za chini katika mtihani, huenda hilo litaamsha fikira zake na atajitayarisha vizuri wakati ujao. Mwana wako akizozana na rafiki yake, mfariji—lakini kwa wakati unaofaa msaidie ajichunguze kwa kujiuliza, ‘Ninapotafakari hali iliyotokea, je, nilichangia kwa njia yoyote mzozano huo?’ Watoto ambao hujifunza kutatua matatizo yao huwa imara na wanajiamini zaidi—sifa ambazo hawatajifunza ikiwa mtu fulani atawatatulia matatizo yao kila wakati.
“Kila mmoja na athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi.”—Wagalatia 6:4

 3 Kuwanunulia Vitu Kupita Kiasi

Tatizo. Katika utafiti uliofanyiwa vijana, asilimia 81 walisema kwamba lengo muhimu sana katika kizazi chao ni ‘kuwa tajiri’—na waliona jambo hilo kuwa muhimu zaidi kuliko kuwasaidia wengine. Lakini kufuatilia utajiri hakumfanyi mtu aridhike. Kwa kweli, utafiti umeonyesha kwamba watu wanaokazia fikira mali hawana furaha sana na wameshuka moyo zaidi. Pia wana uwezekano mkubwa wa kuwa na matatizo ya kimwili na ya kiakili.
Kisababishi ni nini? Katika visa fulani, watoto wanalelewa katika familia zinazofuatilia mali. Kitabu The Narcissism Epidemic kinasema: “Wazazi wanataka kuwafurahisha watoto wao, nao watoto wanataka vitu vya kimwili. Kwa hiyo, wazazi huwanunulia vitu hivyo. Nao watoto wanakuwa na furaha lakini kwa muda mfupi tu. Kisha wanataka vitu zaidi.”
Bila shaka, kupitia matangazo ya kibiashara, wafanyabiashara wametumia vibaya mwelekeo huo wa kupenda kununua vitu. Wameendeleza wazo la kwamba ‘Lazima upate kilicho bora’ na ‘Unastahili kilicho bora.’ Vijana wengi wamepumbazwa na ujumbe huo na sasa wana madeni kwa sababu wameshindwa kulipia vitu hivyo ambavyo eti ‘lazima wavipate.’
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba pesa ni muhimu. (Mhubiri 7:12) Wakati huohuo, inaonya kwamba “Kupenda pesa ni chanzo cha mambo mabaya ya namna zote.” Inaongezea hivi: “Kwa kujitahidi kufikia upendo huo wengine . . . wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.” (1 Timotheo 6:10) Biblia inatutia moyo tusifuatilie utajiri bali turidhike na mahitaji muhimu ya maisha.—1 Timotheo 6:7, 8.
“Wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka katika jaribu na mtego na tamaa nyingi za kijinga na zenye kudhuru.”—1 Timotheo 6:9
Mambo unayoweza kufanya. Ukiwa mzazi, chunguza mtazamo wako kuelekea pesa na vitu ambavyo unaweza kununua ukiwa na pesa. Tanguliza mambo yanayofaa na uwasaidie watoto wako kufanya hivyo pia. Kitabu Narcissism Epidemic kilichonukuliwa kwenye makala hii kinapendekeza hivi: “Wazazi na watoto wanaweza kuzungumzia mambo kama vile ‘Ni wakati gani ni jambo la hekima kununua vitu vilivyopunguzwa bei? Ni wakati gani si jambo la hekima kufanya hivyo?’ ‘Riba ni nini?’ ‘Ni lini ulinunua kitu fulani kwa sababu tu mtu fulani alikuambia ukinunue?’”
Uwe mwangalifu usitumie vitu vya kimwili kufunika matatizo ya familia ambayo yanapaswa kushughulikiwa. Kitabu The Price of Privilege kinasema hivi: “Kutumia vitu vya kimwili kutuliza matatizo hakutayasuluhisha: matatizo yanahitaji kusuluhishwa kwa kutumia akili, ufahamu, na hisia-mwenzi, si kwa kununua viatu na vibeti.”

Kulea Watoto Wenye Kujali Katika Ulimwengu Wenye Ubinafsi

KILA siku watu hupata fursa nyingi za kuwatendea wengine kwa fadhili. Hata hivyo, inaonekana kwamba watu wengi hujifikiria tu. Unaweza kuona jambo hilo kila mahali—jinsi watu wanavyowapunja wengine bila aibu, jinsi wanavyoendesha magari bila kujali, jinsi wanavyotumia lugha chafu na wanavyolipuka kwa hasira.
Mtazamo wa “mimi kwanza” pia unaonekana katika familia nyingi. Kwa mfano, wenzi fulani hutalikiana kwa sababu tu mwenzi mmoja anahisi anastahili kuwa na mtu bora kuliko yule aliye naye sasa. Bila kujua, wazazi wengine pia wanaweza kukuza mtazamo wa ubinafsi katika watoto wao. Jinsi gani? Kwa kumpa mtoto chochote anachotaka, na kusita kumpa nidhamu yoyote.
Tofauti na hilo, wazazi wengi wanawazoeza watoto wao kutanguliza masilahi ya wengine, na wanapata faida kubwa. Watoto wanaowajali wengine wanaweza kuanzisha na kufurahia urafiki wenye kudumu. Pia wanaweza kuwa na uradhi. Kwa nini? Kwa sababu kama Biblia inavyosema, “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.
Ikiwa wewe ni mzazi, unawezaje kuwasaidia watoto wako wapate faida za kuwa wenye fadhili na waepuke kuathiriwa na mtazamo wa kujifikiria ambao umeenea? Chunguza mambo matatu yanayoweza kumfanya mtoto wako awe na mtazamo wa “mimi kwanza,” na jinsi ambavyo unaweza kuyaepuka.

 1 Kumsifu Mtoto Kupita Kiasi

Tatizo. Watafiti wameona mwelekeo usiofaa: Vijana wengi wanapoanza kufanya kazi wanakuwa na mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu—mtazamo huo unawafanya wadai mafanikio hata ikiwa hawajafanya chochote kustahili mafanikio hayo. Baadhi yao hudhani kwamba watapandishwa cheo haraka, hata kabla ya kuwa stadi katika kazi yao. Wengine wanajiona kuwa bora na kwamba wanastahili kutendewa hivyo—wasipotendewa hivyo, wanashuka moyo.
Kisababishi ni nini? Nyakati nyingine huenda mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu ukatokana na malezi ya mtu. Kwa mfano, wazazi fulani wameathiriwa sana na wazo ambalo limeendelezwa katika miaka ya karibuni kwamba kujiheshimu ndilo jambo muhimu zaidi na linapaswa kuzingatiwa. Ilisemekana kwamba wazo hilo linafaa kwa kuwa ikiwa mtoto anafaidika anaposifiwa kidogo, basi akisifiwa sana atafaidika zaidi. Kwa upande mwingine, ilisemekana kwamba kumwonyesha mtoto kwamba hufurahishwi na mambo anayofanya kutamvunja moyo. Na mzazi aliyefanya hivyo alionwa kuwa mzazi asiyefaa kwani ulimwengu ulikuwa na lengo la kuwafanya watu wajiheshimu. Wazazi waliambiwa kwamba hawapaswi kumfanya mtoto ahisi kuwa amekosea.
Kwa sababu hiyo, wazazi wengi walianza kuwasifu sana watoto wao hata wakati ambapo hawakufanya jambo lolote linalostahili sifa. Mtoto alipotimiza jambo lolote, hata liwe dogo kiasi gani, alisifiwa; alipofanya makosa, hata yawe makubwa kiasi gani, yalipuuzwa. Wazazi waliamini kwamba siri ya kumfanya mtoto ajiheshimu ni kupuuza makosa na kusifu jambo lingine lolote. Kuwafanya watoto wajihisi vizuri kukawa jambo muhimu zaidi kuliko kuwafundisha kujitahidi kutimiza mambo ambayo yatawafanya wajihisi vizuri.
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba mtu anapaswa kusifiwa anapostahili. (Mathayo 25:19-21) Lakini kuwasifu watoto ili tu wajihisi vizuri kunaweza kuwafanya wawe na maoni yasiyofaa kujihusu. Biblia inasema hivi kwa kufaa: “Yeyote akifikiri kuwa yeye ni kitu wakati yeye si kitu, anaidanganya akili yake mwenyewe.” (Wagalatia 6:3) Kuna sababu nzuri kwa nini Biblia inawaambia wazazi: “Usimnyime mvulana nidhamu. Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa.” *Methali 23:13.
Mambo unayoweza kufanya. Fanya iwe lengo lako kumrekebisha mtoto inapohitajiwa na kumsifu anapostahili kikweli. Usiwasifu watoto kwa sababu tu unataka kuwafanya wajihisi vizuri. Huenda hawatafaidika. Kitabu Generation Me kinasema: “Mtu hujiheshimu kikweli kwa sababu ya kuboresha vipawa vyake na kujifunza mambo, hajiheshimu kwa sababu tu ya kusifiwa bila sababu.”
“Msijifikirie kuwa watu wa juu kuliko mlivyo. Badala yake, muwe na kiasi.”—Warumi 12:3, Neno—Agano Jipya

 2 Kumlinda Kupita Kiasi

Tatizo. Imeonekana kwamba vijana wengi huwa hawajajitayarisha kukabiliana na matatizo wanapoanza kufanya kazi. Wengine huvunjika moyo sana wanapochambuliwa kidogo tu. Wengine hawakubali kufanya kazi yoyote isipokuwa ile inayowapendeza. Kwa mfano, katika kitabu Escaping the Endless Adolescence, Dakt. Joseph Allen anasimulia kuhusu kijana mmoja ambaye alimwambia hivi alipokuwa akimhoji kwa ajili ya kazi fulani: “Ninaona kwamba sehemu fulani za kazi hii zinaweza kunichosha, nami sitaki kuchoka.” Dakt. Allen anaandika hivi: “Inaonekana hakuelewa kwamba kazi zote huwa na mambo fulani yanayochosha. Mtu anawezaje kuwa na umri wa miaka 23 na asijue jambo hilo?”
Kisababishi ni nini? Katika miaka ya hivi karibuni, wazazi wengi wameamua kuwalinda watoto wao kutokana na matatizo ya aina yoyote. Kwa sababu hiyo, binti yao anapopata alama za chini katika mtihani, wazazi huingilia kati na kumlazimisha mwalimu ampe alama za juu. Au, mwana wao anapoharibu kitu fulani anapocheza, wazazi huingilia na kumlipia. Au mwana wao anapozozana na rafiki yake, wazazi humlaumu rafiki yake.
Ingawa ni jambo la kawaida kutaka kuwalinda watoto wako, unapowalinda kupita kiasi unaweza kuwafunza jambo lisilofaa—kwamba hawahitaji kuwajibika kwa matendo yao. “Badala ya kujifunza kwamba wanaweza kukabiliana na uchungu na mambo yanayokatisha tamaa, na kujifunza jambo fulani kutokana nayo,” kinasema kitabu Positive Discipline for Teenagers, “watoto [hao] huwa watu wazima ambao ni wenye ubinafsi sana, wakiwa na maoni ya kwamba kila mtu, kutia ndani wazazi wao, wanapaswa kuwatimizia mahitaji yao.”
Biblia inasema nini? Matatizo ni sehemu ya maisha. Kwa kweli Biblia inasema: “Mambo mabaya huwapata watu wote!” (Mhubiri 9:11, Easy-to-Read Version) Hilo linatia ndani watu wazuri. Kwa mfano, Paulo, mtume Mkristo alivumilia matatizo ya aina mbalimbali alipokuwa akihubiri. Hata hivyo, kukabiliana na matatizo hayo kulimletea faida! Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwa mwenye kujitosheleza katika hali zozote nilizo nazo. . . . Nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kupatwa na uhitaji.”—Wafilipi 4:11, 12.
Mambo unayoweza kufanya. Ukizingatia ukomavu wa watoto wako, jitahidi kufuata kanuni hii ya Biblia: “Kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) Mwana wako akiharibu kitu fulani anapocheza, ingefaa umwache alipie kitu hicho. Binti yako akipata alama za chini katika mtihani, huenda hilo litaamsha fikira zake na atajitayarisha vizuri wakati ujao. Mwana wako akizozana na rafiki yake, mfariji—lakini kwa wakati unaofaa msaidie ajichunguze kwa kujiuliza, ‘Ninapotafakari hali iliyotokea, je, nilichangia kwa njia yoyote mzozano huo?’ Watoto ambao hujifunza kutatua matatizo yao huwa imara na wanajiamini zaidi—sifa ambazo hawatajifunza ikiwa mtu fulani atawatatulia matatizo yao kila wakati.
“Kila mmoja na athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi.”—Wagalatia 6:4

 3 Kuwanunulia Vitu Kupita Kiasi

Tatizo. Katika utafiti uliofanyiwa vijana, asilimia 81 walisema kwamba lengo muhimu sana katika kizazi chao ni ‘kuwa tajiri’—na waliona jambo hilo kuwa muhimu zaidi kuliko kuwasaidia wengine. Lakini kufuatilia utajiri hakumfanyi mtu aridhike. Kwa kweli, utafiti umeonyesha kwamba watu wanaokazia fikira mali hawana furaha sana na wameshuka moyo zaidi. Pia wana uwezekano mkubwa wa kuwa na matatizo ya kimwili na ya kiakili.
Kisababishi ni nini? Katika visa fulani, watoto wanalelewa katika familia zinazofuatilia mali. Kitabu The Narcissism Epidemic kinasema: “Wazazi wanataka kuwafurahisha watoto wao, nao watoto wanataka vitu vya kimwili. Kwa hiyo, wazazi huwanunulia vitu hivyo. Nao watoto wanakuwa na furaha lakini kwa muda mfupi tu. Kisha wanataka vitu zaidi.”
Bila shaka, kupitia matangazo ya kibiashara, wafanyabiashara wametumia vibaya mwelekeo huo wa kupenda kununua vitu. Wameendeleza wazo la kwamba ‘Lazima upate kilicho bora’ na ‘Unastahili kilicho bora.’ Vijana wengi wamepumbazwa na ujumbe huo na sasa wana madeni kwa sababu wameshindwa kulipia vitu hivyo ambavyo eti ‘lazima wavipate.’
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba pesa ni muhimu. (Mhubiri 7:12) Wakati huohuo, inaonya kwamba “Kupenda pesa ni chanzo cha mambo mabaya ya namna zote.” Inaongezea hivi: “Kwa kujitahidi kufikia upendo huo wengine . . . wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.” (1 Timotheo 6:10) Biblia inatutia moyo tusifuatilie utajiri bali turidhike na mahitaji muhimu ya maisha.—1 Timotheo 6:7, 8.
“Wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka katika jaribu na mtego na tamaa nyingi za kijinga na zenye kudhuru.”—1 Timotheo 6:9
Mambo unayoweza kufanya. Ukiwa mzazi, chunguza mtazamo wako kuelekea pesa na vitu ambavyo unaweza kununua ukiwa na pesa. Tanguliza mambo yanayofaa na uwasaidie watoto wako kufanya hivyo pia. Kitabu Narcissism Epidemic kilichonukuliwa kwenye makala hii kinapendekeza hivi: “Wazazi na watoto wanaweza kuzungumzia mambo kama vile ‘Ni wakati gani ni jambo la hekima kununua vitu vilivyopunguzwa bei? Ni wakati gani si jambo la hekima kufanya hivyo?’ ‘Riba ni nini?’ ‘Ni lini ulinunua kitu fulani kwa sababu tu mtu fulani alikuambia ukinunue?’”
Uwe mwangalifu usitumie vitu vya kimwili kufunika matatizo ya familia ambayo yanapaswa kushughulikiwa. Kitabu The Price of Privilege kinasema hivi: “Kutumia vitu vya kimwili kutuliza matatizo hakutayasuluhisha: matatizo yanahitaji kusuluhishwa kwa kutumia akili, ufahamu, na hisia-mwenzi, si kwa kununua viatu na vibeti.”
(Source: JW)
Saved under :

No comments:

Leave a Reply