Kwanza, tambua kwamba matineja wanahitaji—na
hata
wanataka sana
—kuwekewa mipaka. Kwa hiyo
weka
sheria, na uhakikishe kwamba kijana wako anazielewa. Kitabu
Letting
Go With Love and Confidence kinasema hivi, “Vijana wanaobalehe wanapowekewa
mipaka iliyo wazi na kutazamia wazazi wawape mwongozo fulani, ni vigumu kwao
kujiingiza katika tabia zisizofaa.” Kinyume cha hilo, wazazi ambao huhisi kwamba
hakuna uhitaji wa kuweka sheria huwafanya vijana wao wafikiri kwamba wazazi wao
hawajali. Na kwa hakika jambo hilo huwafanya waasi.
—Kanuni ya Biblia:
Methali 29:15.
Unawezaje kuonyesha usawaziko?
Acha
kijana wako aeleze anavyohisi kuhusu sheria za familia. Kwa mfano,
ikiwa anaomba muda aliyowekewa wa kurudi nyumbani urekebishwe,
msikilize
anapoeleza sababu zake. Huenda ikawa rahisi zaidi kwa tineja kuheshimu
na kufuata maamuzi unayofanya—hata kama hakubaliani nayo—ikiwa anahisi kwamba
umemsikiliza kwa makini.
— Kanuni ya Biblia: Yakobo 1:19.
Hata
hivyo, kabla ya kufanya maamuzi kumbuka jambo hili: Matineja huwa na mwelekeo wa
kutaka uhuru zaidi kuliko wanavyostahili, na wakati huohuo wazazi huenda wakawa
na mwelekeo wa kuwapa matineja uhuru kidogo kuliko wanavyopaswa kuwapa. Kwa
hiyo,
fikiria kwa uzito ombi la kijana wako. Je, ameonyesha
kuwa anaweza kutegemeka? Je, sheria inaweza kubadilishwa kwa sababu ya hali?
Inapofaa, uwe tayari kubadilikana kulingana na hali.
—Kanuni ya Biblia:
Mwanzo
19:17-22.
Mbali
na kusikiliza hisia za kijana wako, hakikisha pia
yeye anajua mahangaiko
yako kumhusu. Kwa kufanya hivyo, unamfundisha kutofikiria
mapendezi yake tu bali pia afikirie hisia za wengine.—
Kanuni ya Biblia:
1 Wakorintho 10:24.
Mwishowe,
fanya uamuzi na ueleze
sababu za uamuzi huo. Hata kama hapendezwi na uamuzi huo, yaelekea
atafurahi kuwa na wazazi wanaomsikiliza na kutaka kujua maoni yake. Kumbuka,
unamfundisha kijana wako anayebalehe kutenda kama mtu mzima. Kwa kumwekea kijana
wako sheria zinazofaa na kuzizungumzia pamoja naye, utamsaidia awe mtu mzima
mwenye kutegemeka.
—Kanuni ya Biblia: Methali
22:6.
No comments: