Written by Anonymous

HAPPY NEW YEAR 2015

by Anonymous / 06 Jan 2015

...

Written by Anonymous

MERY CHRISTMAS

by Anonymous / 25 Dec 2014

WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRISTMAS WE WISH U A MERY CHRIS...

Written by Anonymous

HAMUGEMBE PRAISE AND WORSHIP TEAM KUZINDUA ALBUM YAO MWEZI APRIL

by Anonymous / 31 Mar 2014

 Kikundi cha Hamugembe Praise and Worship Team cha mjini Bukoba  kinatarajia kuzindua album yao ya nyimbo za kusifu na kuabudu ...

Written by Anonymous

WE WISH YOU A HAPPY NEW YEAR 2014

by Anonymous / 31 Dec 2013

Leo ndio siku ya mwisho kwa mwaka huu 2013 na masaa machache yajayo tutaingia mwaka ujao 2014.Mtandao huu unawatakia kila la kheri na ba...

Written by Anonymous

KWAYA KUU YA USHARIKA WA AZANIA FRONT NDIO MABINGWA WA UIMBAJI WA K.K.K.T – DMP

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

Written by Anonymous

MASHINDANO YA UIMBAJI KWAYA KUU NGAZI YA DAYOSISI YA KANISA LA K.K.K.T (DMP) YAFANA USHARIKA WA MBEZI BEACH LEO

by Anonymous / 26 Oct 2013

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

KUTOKA MADHABAHUNI

IBADA KATIKA KANISA LA LIVING WATER CENTER MAKUTI KAWE JUMAPILI HII

Jumapili hii ilifanyoka ibada nzuri katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe ambapo kiongozi wa kanisa hilo Mtume Onesmo Ndegi  (pichani juu) aliongoza na kuhubiri Pichani juu Mtume Onesmo Ndegi akimtambulisha ndugu wa m...

More KUTOKA MADHABAHUNI
More NENO LA LEO
More MAHUBIRI
More MAOMBI

HABARI ZA KIDINI

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MHESHIMIWA MAKONDA AZINDUA VITABU VYA INJILI KANISA LA LIVING WATER CENTER KAWE KAWE

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mheshimiwa Paul Makonda jumapili hii alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa vitabu vya injili vya mwalimu Lilian Ndegi katika kanisa la Living Water Center - Makuti Kawe Bwana Makonda (pichani juu) alimsh...

More HABARI ZA KIDINI

More HABARI ZA KIDINI

KIJANA ANAWEZAJE KUTHIBITI HASIRA YAKE?

Posted by : Unknown on : Tuesday, April 21, 2015 0 comments
Unknown
Saved under :



 Maswali

  • Unakasirika mara nyingi kadiri gani?
    • mara chache sana
    • pindi fulani
    • kila siku
  • Hasira yako ni kali kadiri gani?
    • kiasi
    • kali
    • kali sana
  • Ni nani ambaye mara nyingi hukukasirisha?
    • mzazi
    • mdogo wako
    • rafiki
Ikiwa unaona unahitaji kudhibiti hasira yako, makala hii itakusaidia! Kwanza, fikiria baadhi ya sababu za kubaki ukiwa mtulivu unapochokozeka.

 Kwa nini ni muhimu

Afya yako. Methali 14:30 inasema hivi: “Moyo mtulivu ni uzima wa mwili wenye nyama.” Kinyume na hilo, gazeti la Journal of Medicine and Life linasema kwamba “hasira inaweza kuathiri moja kwa moja magonjwa ya moyo.”
Rafiki zako. Biblia inasema hivi: “Usishirikiane na mtu yeyote mwenye mazoea ya kukasirika; wala usiende pamoja na mtu wa mifoko ya ghadhabu.” (Methali 22:24) Hivyo, ikiwa una tatizo la kudhibiti hasira yako, usishangae watu wakikuepuka. Mwanamke kijana anayeitwa Jasmine, anasema hivi: “Usipojifunza kudhibiti hasira yako, hutakuwa na marafiki.”
Sifa yako. Ethan, mwenye umri wa miaka 17, anasema hivi: “Usipodhibiti hasira yako, wengine watatambua hilo na watakuwa na maoni yasiyofaa kukuelekea.” Jiulize hivi, ‘Ningependa watu wanioneje—nikiwa mtu wa kufanya amani kwa utulivu au mtu anayelipuka kwa hasira wakati wowote?’ Biblia inasema hivi: “Yule ambaye si mwepesi wa hasira ana utambuzi mwingi, lakini anayekosa subira anainua upumbavu.”Methali 14:29.
Rafiki za mvulana tineja wanaondoka anaposhindwa kudhibiti hasira yake
Hakuna mtu anayependa kuwa karibu na mtu mwenye milipuko ya hasira

 Unachoweza kufanya

Fikiria maandiko na maelezo yafuatayo, kisha ujiulize maswali yanayofuata.
  • Methali 29:22: “Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, na mtu yeyote mwenye mwelekeo wa ghadhabu ana makosa mengi.”
    “Ilikuwa vigumu sana kwangu kudhibiti hasira nilipokuwa tineja. Watu wa ukoo wa upande wa baba wana tatizo hilohilo. Sisi huuita udhaifu wa kuzaliwa. Ni vigumu sana kwetu kudhibiti hasira!”—Kerri.
    Je, mimi ni mwenye hasira? Ikiwa ninakubali kuwa nimesitawisha sifa nzuri, je, inapatana na akili kutetea kwamba kushindwa kudhibiti hasira ni udhaifu wa kuzaliwa?
  • Methali 15:1: “Jibu, linapokuwa la upole, hugeuza ghadhabu, lakini neno linaloumiza hufanya hasira ipande.”
    “Siri ni kujifunza kudhibiti hisia zako. Ukisitawisha sifa ya upole na kuzingatia sifa nzuri, kudhibiti hasira hakutakuwa tatizo tena.”—Daryl.
    Kwa nini ni muhimu kuzingatia ninavyoitikia ninapochokozeka?
  • Methali 26:20: “Pasipo na kuni moto huzimika.”
    “Kwa kawaida ninapoitikia kwa fadhili, hilo humtuliza mtu yule mwingine na tunaweza kuwasiliana kwa utulivu.”—Jasmine.
    Maneno au matendo yangu yanawezaje kuongezea kuni kwenye moto?
  • Methali 22:3: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha, lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.”
    “Wakati mwingine ninahitaji tu kuondoka mahali hapo ili nipate muda wa kufikiria kilichotukia, kisha ninaweza kushughulika na jambo hilo baada ya kutulia.”—Gary.
    Ni wakati gani unaofaa kuondoka mahali mlipo bila kumfanya mwenzako ahisi kana kwamba unampuuza?
  • Yakobo 3:2: “Kwa maana sisi sote hujikwaa mara nyingi.”
    “Tunapaswa kujutia makosa yetu, hata hivyo, tunapaswa kujifunza kutokana nayo pia. Tunapaswa kuinuka tena tunapojikwaa na kuazimia kushughulikia hali vizuri zaidi wakati ujao.”—Kerri.
Dokezo: Jiwekee lengo. Azimia kubaki ukiwa mtulivu kwa kipindi fulani cha wakati—labda kwa mwezi mmoja. Weka rekodi ya maendeleo unayofanya.

(Source: www.jw.org)

No comments:

Leave a Reply