Latest News


More

KWAYA KUU YA MAGOMENI YAIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA UIMBAJI JIMBO LA KASKAZANI

Posted by : Unknown on : Sunday, October 20, 2013 0 comments
Unknown


Kwaya kuu ya Usharika wa Kinondoni ndio mabingwa wa uimbaji wa jimbo la Kaskazini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Mashariki na Pwani
Akitangaza matokeo hayo Mchungaji mkuu wa jimbo na mchungaji kiongozi wa Usharika waMbezi Beach mchungaji Anta Muro alisema kwaya kuu ya Usharika wa Magomeni imeibuka washindi baada ya kupata alama 87.47
Wakitoa maoni yao kabla ya kutangazwa kwa matokeo hayo majaji walioongoza mashindano hayo walisemavikundi vyote vimeimba kwa ustadi na weledi mkubwa
Baadhi ya maoni waliotoa ambayo wamesema yanafaa kudumishwa ni;
1.Kwaya zote zilivaa sare kama vilivyoambiwa na walipendeza sana
2.Uimbaji mzuri  na utulivu ulizingatiwa
3.Waandishi wa muziki wa vikundi vyote  walichapa miziki yao
4.Nyimbo za kiutamaduni zilikua za mtandao wa kitaifa .Karibu kila upande wa Tanzania uliwakilishwa
5.Baadhi ya vikundi haswa chaguo la kwaya walitunga nyimbo zao wenyewe.ali hiyo iendelee na sio kutegemea nyimbo za watu wengine
Mambo ambayo wanatakiwa wanakwaya na waalimu waboreshe
1.Note ziimbwe kwa thamani zake zisikatwe katwe
2.Vikubdi karibu vyote sauti ya kwanza ina nguvu sana.Hivyo ziimbwe vizuri ili sauti nyingine nazi zisikike
3.Dynamics zifuatwe jinsi zilivyoandikwa .walimu awe mjanja wa kuzifahamu nyimbo
4.Uandishi wa Note uzingatiwe utaalam wa maandishi
5.Matendo yanayofanyika jukwaani yawiane  na ujumbe wa nyimbo
6.Matamshi ya maneno: Mfano Dunia usiseme  Duni a matamshi yaendane na neon husika
7.Makondakta – alama za mwiho zisitumike na waalimu kama hazipo kwenye note
8.Viongozi wanaoongoza (condactor) wawe chacu, kwani hii ni sanaa, hivyo inabidi wawe wabunifu wa kutawala jukwaa
Mashindano hayo yaliratibiwa na majaji watatu   wakiwepo mchungaji Kijalo , ndugu Gaitan na ndugu Edwirn Andarson

Kiongozi wa kwaya ya Usharika wa Mbezi Beach ambao walichukua ushindi wa tatu akipokea kikombe kwa mkuu wa jimbo mchungaji Muro


Mwalimu kiongozi wa kwaya ya Usharika wa Kinondoni  (Mwalimu Lwiza) ambao walichukua ushindi wa pili akipokea kikombe kwa mkuu wa jimbo mchungaji Muro

Kiongozi wa kwaya ya Usharika wa Magomeni  ambao walichukua ushindi wa kwanza  akipokea kikombe kwa mkuu wa jimbo mchungaji Muro.Mwalimu huyu ni ndugu na mwalimu wa kwaya ya Kinondoni


Kamisaa alikua mchungaji Mwaipopo
Washindi wa pili ni kwaya ya Usharika wa Kinondoni ambayo imepata alama 87.22 na mshindi wa tatu ni kwaya ya Usharika wa Mbezi Beach ambayo ilipata alama 87.08
Jumla ya kwaya 11 zilishindana na kwaya nyingine na alama walizopata ni kama ifuatavyo;
Kwaya kuu ya Usharika wa Msasani alama 82.6
Kwaya kuu ya Usharika wa Manzese alama 79
Kwaya ya kuu Usharika wa Wazo Hill alama 81.97
Kwaya ya kuu usharika wa Sinza alama 82.38
Kwaya ya kuu Usharika wa Kunduchi Beach alama 81.95
Kwaya kuu ya  Usharika wa Bubju A alama 79.94
Kwaya kuu ya Usharika wa Kijitonyama alama 85.22
Kwaya kuu ya Usharika wa Ubungo alama 82.11


Kwaya ya Usharika wa Magomeni wakiimba kwenye mashindano hayo,
Kwaya hii inaongozwa na mwalimu Erick Lwiza

 Washindi wa Pili kwaya  kuu ya Usharika wa Kinondoni wakiimba kwenye mashindano hayo
Mwalimu wa kwaya hii ni mwalimu Kennedy Lwiza ambaye ni ndugu na mwalimu wa kwaya ya Usharika wa Magomeni ambao walichukua ushindi wa Kwanza
Hongera familia ya Lwiza kwa kumwimbia Mungu kwa ustadi


 Kwaya kuu ya Usharika wa Mbezi beach ambao walichukua ushindi wa tatu

Mgeni rasmi mchungaji Muro ambaye pia ni mkuu wa jimbo la kaskazini akimpongeza kamisaa wa mashindano hayo mchungaji Mwaipopo kwa kazi nzuri walioifanya ya uamuzi

"Blog hii inawatakia  kila la kheri wawakilishi hawa wa jimbo la kaskazini katika mashindano ya Dayosisi jumamosi ijayo huko kwenye usharika wa Mbezi Beach"

No comments:

Leave a Reply