Latest News


More

WANAUME WAKIMBIA TOHARA NCHINI KENYA

Posted by : Unknown on : Tuesday, August 12, 2014 0 comments
Unknown
Saved under :
Wanaume wanaokwepa kutahiriwa wajikuta taabani kwa kufanyiwa kitendo hicho kwa lazima Kenya
Nchini Kenya ambapo wanaume kutoka kabila la Turkana na makabila mengine ambayo hayana utamaduni wa kutahiri wanaume sasa wanaishi kwa hofu baada ya baadhi yao kutahiriwa kwa lazima.
Vijana kutoka kabila la Bukusu wamekuwa wakiwavamia wanaume ambao hawajatahiriwa katika mji wa Moi's Bridge na kuwapaka matope na maji taka na kisha kuwatahiri hadharani kando ya barabara .
Wabukusu huchukulia mtu asiyetahiriwa kuwa mchafu na mwoga, lakini wanaume wanaotahiriwa bila ridhaa yao wanalalamika kuwa wanatwikwa utamaduni usio wao.
Odeo Sirari ambaye yupo katika mji huo wa Moi's Bridge amekutana na vijana hao na kutuandalia taarifa ifuatayo.
Saved under :

No comments:

Leave a Reply