Latest News


More

NDOA MBILI ZA PAMOJA ZAFUNGWA LEO KANISA LA K.K.K.T -USHARIKA WA MWENGE

Posted by : Unknown on : Sunday, December 7, 2014 0 comments
Unknown
Saved under : ,
 Leo katika kanisa la K.K.K.T Usharika wa Mwenge zimefungwa ndoa mbili za pamoja
Katika ibada hiyo ambayo pia ilikua ni ibada ya familia ilishuhudiwa ndoa mbili zikifungwa na baada ya kufungwa washarika wote waliohudhuria ibada hiyo, maharusi pamoja na ndugu , jamaa na marafiki zao walishiriki chakula cha mchana ambacho kiliandaliwa na Usharika huo
Ibada hiyo iliongozwa na mchungaji kiongozi wa Usharika wa Mwenge mchungaji Kaanasia Msangi huku mahubiri yakitolewa na mchungaji Ernest Kadiva toka ofisi kuu ya Dayosisi ya Mashariki na Pwani
Pichani juu kwaya ya Uinjilisti ya Usharika wa Sinza ikihudumu kwenye ibada hiyo
 Maharusi wakipata baraka toka kwa mchungaji Kadiva
Maharusi wakiwa kwenye ibada ya ndoa


Maharusi (chini na juu) wakila viapo mbele ya Usharika

 Maharusi wakila kiapo kanisani hapo
 Baada ya ibada iliandaliwa hafla ya kukata na shoka kanisani hapo ambapo washarika wote , ndugu jamaa na marafiki wa maharusi walihudhuria
Pichani juu ni maharusi wakiwa kwenye hafla hiyo
 Mc akiwapa mkono maharusi kwenye hafla hiyo
 Mchungaji kiongozi wa Usharika wa Mwenge Kaanasia Msangi akiwa na mumewe mzee Msangi kulia.Katikati ni mke wa Mchungaji Kadiva( anayesoma gazeti) pembeni kushoto ni mfanyakazi  toka Dayosisi ambaye jina lake halikufahamika mara moja
 Wageni wakipata vinywaji kwenye sherehe hiyo ambayo ilifanyika kanisani hapo
 Ulifika wakati wa kufungua shampaigne, hakika ilikua ni furaha ilioje
 Maharusi wakiwa kwenye picha ya pamoja na wapambe wao


 Picha ya pamoja kati ya maharusi na waimbaji wa kwaya kuu ya Usharika wa MwengeMaharusi ni waimbaji wa kwaya ya Uinjilisti ya Usharika wa Mwenge
Picha ya pamoja ya maharusi na viongozi wa Usharika wa Mwenge pia viongozi wa dayosisi waliokuwepo kwenye hafla hiyo.Hakika ilipendeza

No comments:

Leave a Reply