Latest News


More

TUNAWEZAJE KUMKUMBUKA BWANA YESU KRISTO?

Posted by : Unknown on : Thursday, May 21, 2015 0 comments
Unknown
Saved under :

Yesu Kristo—Tumkumbuke kwa Njia Gani?

Mwezi wa Desemba watu wengi ulimwenguni pote huona picha za Yesu akiwa mtoto. Akiwa amelazwa kwenye hori, yaani, sanduku kubwa linalotumiwa kulishia wanyama. Lakini je, tunapaswa kumkumbuka Yesu akiwa mtoto tu? * Acheni tuzungumzie njia muhimu zaidi ya kumkumbuka. Tunaweza kujifunza kutokana na jambo lililowapata wachungaji waliokuwa malishoni karibu na Bethlehemu usiku mmoja.
Ghafula malaika anawatokea wachungaji hao. Anawaambia hivi: “Mwokozi ambaye ni Kristo Bwana, amezaliwa kwenu.” Pia, malaika anawaambia watampata Yesu “akiwa amefungwa vitambaa na akiwa amelala katika hori.” Papo hapo, malaika wengine wengi wanatokea na kuanza ‘kumsifu Mungu.’
Ungehisije kama ungewasikia malaika wakimsifu Mungu?— Wachungaji wanafurahi sana! Wanasema: “Na twende moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukaone jambo hili ambalo limetendeka.” Wanapofika huko wanamkuta “Maria na vilevile Yosefu, na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori.”
Baadaye watu wengine wanakuja Bethlehemu ambako Maria na Yosefu wanakaa. Wachungaji wanapowaambia kuhusu kilichotukia, wote wanashangaa. Je, unafurahi kujua mambo hayo yenye kustaajabisha?— Watu wanaompenda Mungu wanafurahi kuyajua. Sasa acheni tuone ni kwa nini watu wanafurahi sana baada ya Yesu kuzaliwa. Ili tuelewe jambo hilo, tutachunguza mambo yaliyotukia kabla Maria hajaolewa.
Siku moja malaika anayeitwa Gabrieli anamtembelea Maria. Anamwahidi kwamba atazaa mtoto ambaye “atakuwa mkuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi.” Pia, Gabrieli anasema: “Atatawala akiwa  mfalme . . . na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”
Maria anataka kujua hilo litawezekanaje kwa kuwa hajawahi kulala na mwanamume. Basi, Gabrieli anamfafanulia: “Nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika,” na “kile kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.” Huo ungekuwa muujiza mkubwa! Kuuhamisha uhai wa Mwana wa Mungu kutoka mbinguni na kuuweka ndani ya tumbo la uzazi la Maria.
Je, umewahi kuona picha zinazoonyesha wanaume watatu wenye hekima pamoja na wachungaji wakimtembelea mtoto Yesu?— Ni jambo la kawaida kuona picha hizo wakati wa Krismasi. Lakini hazionyeshi jambo sahihi. Wanaume hao watatu walikuwa wanajimu, walizoea kufanya jambo ambalo Mungu alikataza. Acheni tuone kilichotukia walipofika. Biblia inasema: “Walipoingia ndani ya ile nyumbawakamwona huyo mtoto mchanga pamoja na Maria mama yake.” Wakati huo Yesu hakuwa mtoto aliyetoka tu kuzaliwa ndani ya hori; bali alikuwa akiishi pamoja na Yosefu na Maria katika nyumba!
Wanajimu walimpataje Yesu?— Ile “nyota” haikuwaongoza kwenda Bethlehemu kwanza, bali iliwaelekeza kwa Mfalme Herode huko Yerusalemu. Biblia inasema Herode alitaka kumpata Yesu ili amuue. Sasa fikiria jambo hili. Unafikiri ni nani aliyetumia kitu kilichofanana na nyota kuwaongoza wale wanajimu kwa Herode?— Si Yehova, Mungu wa kweli, bali ni mpinzani na adui yake, Shetani Ibilisi!
Leo, Shetani anawafanya watu wamfikirie Yesu kuwa mtoto aliyetoka tu kuzaliwa. Lakini Malaika Gabrieli alimwambia hivi Maria: “[Yesu] atatawala akiwa mfalme . . . , na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” Sasa anatawala akiwa Mfalme huko mbinguni, na hivi karibuni atawaangamiza adui wote wa Mungu. Hilo ndilo jambo tunalopaswa kukumbuka kumhusu Yesu, na tunapaswa kuwaambia wengine kulihusu.
(Source:www.jw.org)

No comments:

Leave a Reply