Latest News


More

JE NISALI AU KUOMBA KUHUSU NINI?

Posted by : Unknown on : Tuesday, October 22, 2013 0 comments
Unknown
Saved under : ,

Je Nisali Kuhusu Nini?
Jibu la Biblia

Unaweza kusali kuhusu jambo lolote linalopatana na matakwa ya Mungu yanayotajwa katika Biblia. “Hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake [Mungu], yeye hutusikia.” (1 Yohana 5:14) Je, unaweza kutaja mambo yanayokuhangaisha? Biblia inasema: “Mimineni moyo wenu mbele zake [Mungu].”—Zaburi 62:8.
Mifano ya mambo unayoweza kusali

Imani katika Mungu.—Luka 17:5.

Roho takatifu, au nguvu za utendaji za Mungu, zikusaidie kutenda yaliyo sawa.—Luka 11:13.
Nguvu za kukabiliana na matatizo na kushinda kishawishi.—Wafilipi 4:13.
Amani ya moyoni, au utulivu.—Wafilipi 4:6, 7.
Hekima ya kufanya maamuzi yanayofaa.—Yakobo 1:5.
Msaada wa kupata mahitaji ya kila siku.—Mathayo 6:11.
Msamaha wa dhambi.—Mathayo 6:12.

No comments:

Leave a Reply