Latest News


More

WANANDOA WAKUMBUSHANA SIKU ZA HARUSI ZAO KWA KULISHANA KEKI KATIKA KANISA LA K.K.K.T USHARIKA WA MWENGE

Posted by : Unknown on : Sunday, January 19, 2014 0 comments
Unknown
Jumapili ya leo katika kanisa la K.K.K.T Usharika wa Mwenge kumefanyika ibada nzuri ambayo imegawanywa katika makundi makuu manne
Ibada ya kwanza ilikua ya wanafamilia wote wakati ibada ya pili ilikua ni maalum kwa watu walio kwenye ndoa.Ibada ya tatu ilikua ya wajane na wagane wakati ibada ya nne ilikua ya vijana peke yao

Ibada hiyo iliyoongozwa na mchungaji kiongozi wa Usharika wa Mwenge mchungaji Kaanasia Msangi na neno lilifundishwa na mchungaki Enock Kagya
Baada ya mahubiri wanandoa walipata nafasi ya kulishana keki kwa wale waliokuja na wenzi wao na wale ambao hawakuja na wenzi wao walilishwa keki na wachungaji waliokuwepo madhabahuni
Hakika ilikua ni siku nzuri kwani wanandoa wengine wana miaka zaidi ya thelathini na walikumbushana siku yao walipofunga ndoa
Pichani juu mchungaji Kaanasia Msangi akibariki keki hizo tayari ziweze kuliwa

 Bwana na Bi Kileo wakikata kata keki tayari kuliwa na wanandoa waliohudhuria ibada hiyo
Bwana Kileo akimlisha mkewe Beatrice ikiwa wakiwa ni wanandoa wa kwanza kufungua zoezi hilo la kulishana keki
 Hawa ndio walionunua hizo keki tatu na kuzitoa ziliwe na wanandoa wote waliohudhuria ibada hiyo
Kutoka kushoto ni Bwana na Bi Chonjo, Bwana na Bi Kileo,Bwana Mushi Benn  Bwana na Bi Severe na bwana na Bi Uronu
Mzee Uronu akimlisha mkewe keki

 Mzee Beny Mushi akilishwa keki na mchungaji
Mzee Severe akilishana keki na mkewe.Hakika iilikua siku ya furaha kwa wanandoa hawa

 Mzee Chonjo akimlisha keki mkewe
 Bwana Isaya akilishana keki na mkewe



 Mzee Rogathe Mushi wakilishana keki na mkewe
 Wanandoa wakiwa wamejiandaa kwenda kulishana keki










 Baada ya ibada wanandoa walipata nafasi ya kupata picha ya pamoja kama inavyoonekana juu na chini

No comments:

Leave a Reply