Latest News


More

Posted on : Saturday, September 5, 2015 [0] comments Label:

ATUPWA JELA KWA KUKATAA KUSAINI CHETI CHA NDOA YA JINSIA MOJA

by : Unknown

Kim Davies aliyekataa kusaini cheti cha ndoa Kentucky

Jaji mmoja nchini Marekani, ameagiza afisa mmoja wa serikali katika jimbo la Kentucky, kufungwa jela, baada ya kukataa kutekeleza agizo la mahakama la kutoa cheti rasmi cha ndoa, kwa wapenzi wawili wa jinsia moja.
Kim Davies amesema imani yake kama Mkristo, haimruhusu kusaini cheti kama hicho. Ndoa ya jinsia moja ilihalalishwa nchini Marekani Juni mwaka huu.
Umauzi huo wa Davis, wa kutosaini cheti hicho umepokelewa kwa hisia tofauti.
Kuna baadhi ya wale wanaomuona kama shujaa huku wengine wakisema ni msaliti.

Tofauti za imani

Davis ambaye ni karani wa mahakama, alikataa kutoa cheti hicho, kwa wanandoa hao katika kaunti ya Rowan iliyoko Kentucky.
Afisa huyo ambaye alichaguliwa na raia amesama, kitendo hicho kinakiuka maadili ya kidini.
Davis sasa ametupwa jela na jaji huyo kwa kudharau mahakama.
Amesema alikuwa amekula kiapo cha kuwa offisini na viapo vina maana nyingi.
Watu wanaoshabikia ndoa ya jinsia moja, walikusanyika nje ya mahakama, wakiimba kuwa mapenzi imeshinda na kusema kuwa sasa wanafuraha kwa sababu wanaweza kufunga ndoa.
Lakini kwa upande wake Kim Davis amepata uungwaji mkono kutoka kwa Wakristo wahafidina na baadhi ya wagombea wa urais wa chama cha Republican, ambao wanasema kuwa Davis amehukumiwa jela kwa kufuata imani zake.
Posted on : Tuesday, April 21, 2015 [0] comments Label: ,

MAMBO YA KUZINGATIA KWA KIJANA ANAYETAKA KUFUNGA NDOA

by : Unknown




Ili uweze kujibu swali hilo, unahitaji kujielewa vizuri. Kwa mfano, fikiria mambo yafuatayo:

Mahusiano

Wewe huwatendeaje wazazi wako na ndugu na dada zako? Je, mara nyingi wewe hushindwa kujizuia unapokuwa nao, labda hata kuzungumza kwa ukali au kwa kejeli? Wao wangejibuje ikiwa wangeulizwa swali hilo kukuhusu? Jinsi unavyoshughulika na watu wa familia yako huonyesha jinsi utakavyomtendea mwenzi wako.Waefeso 4:31.

Mtazamo

Je, wewe huwa na mtazamo mzuri au mbaya kuelekea mambo? Je, wewe hukubali maoni ya wengine, au nyakati zote wewe husisitiza mambo yafanywe kwa njia fulani—njia ile wewe unataka? Je, unaweza kuendelea kuwa mtulivu unapokabili hali ngumu? Je, wewe ni mwenye subira? Kusitawisha sifa za tunda la roho ya Mungu sasa kutakusaidia kujitayarisha kwa ajili ya kuwa mume au mke wakati ujao.Wagalatia 5:22, 23.

Gharama

Wewe hushughulikia pesa kwa njia gani? Je, mara nyingi wewe hujikuta ukiwa na madeni? Je, unaweza kudumisha kazi? Ikiwa huwezi, sababu ni nini? Je, tatizo ni kazi yenyewe? Je, tatizo ni mwajiri? Au je, ni kwa sababu ya zoea au tabia fulani unayohitaji kufanyia kazi? Ikiwa ni vigumu kwako kushughulikia gharama zako mwenyewe, utashughulikiaje za familia yako?1 Timotheo 5:8.

Hali ya Kiroho

Ikiwa wewe ni Shahidi wa Yehova, una sifa gani za kiroho? Je, wewe husoma Neno la Mungu, kushiriki katika huduma, na kutoa maelezo katika mikutano ya Kikristo? Yule utakayefunga ndoa naye anastahili kuwa na mwenzi mwenye nguvu kiroho.Mhubiri 4:9, 10.

Kadiri unavyojielewa, ndivyo utakavyoweza kumpata mtu atakayekusaidia kukuza sifa zako nzuri badala ya udhaifu wako
Posted on : [0] comments Label:

JINSI YA KUSHINDA KINYONGO

by : Unknown

Mke aliyemwekea kinyongo mume wake

KIKWAZO

Unashindwa kusahau mambo mabaya ambayo mwenzi wako alisema au kutenda; maneno yake makali na matendo ya kutojali yamebaki akilini mwako. Hivyo, badala ya kuwa na upendo umekuwa na kinyongo. Inaonekana kwamba huwezi kufanya lolote ila tu kuvumilia ndoa isiyo na furaha. Hilo pia linafanya uwe na kinyongo na mwenzi wako.
Uwe na hakika kwamba unaweza kurekebisha hali hii. Hata hivyo, kwanza chunguza mambo machache kuhusu kinyongo.

UNACHOPASWA KUJUA

Mume na mke wakiwa kwenye baiskeli iliyozuiwa na nanga
Kuweka kingyongo husababisha kikwazo kinachozuia ndoa yako kusonga mbele
Kinyongo kinaweza kuharibu ndoa. Kwa nini? Kwa sababu kinadhoofisha sifa ambazo ni msingi wa ndoa, kama vile upendo, uaminifu, na ushikamanifu. Hivyo basi, kinyongo si kisababishi cha matatizo ya ndoa, bali kinyongo ni tatizo la ndoa. Kwa kufaa Biblia hutushauri tuondolee mbali “uchungu wote wenye uovu.”—Waefeso 4:31.
Ukiwa na kinyongo, unajiumiza mwenyewe. Kuweka kinyongo ni kama kujipiga kofi na kutarajia mtu mwingine ahisi uchungu. “Huenda mshiriki wa familia ambaye una kinyongo naye anahisi vizuri, anafurahia maisha, na labda hasumbuliwi na hali hiyo,” akaandika Mark Sichel katika kitabu chake Healing From Family Rifts. Somo ni nini? “Kinyongo kinakuumiza kuliko kinavyomuumiza mtu uliyemwekea kinyongo,” anasema Sichel.
Kuweka kinyongo ni kama kujipiga kofi na kutarajia mtu mwingine ahisi uchungu
Wewe ndiye unayeamua kuwa na kinyongo. Watu fulani hawaamini hivyo. Wanasema, ‘Mwenzi wangu ndiye aliyefanya niwe na kinyongo.’ Tatizo ni kwamba mawazo kama hayo yanakazia jambo ambalo haliwezi kudhibitiwa, yaani, matendo ya mtu mwingine. Biblia inatoa suluhisho. Inasema hivi: “Kila mmoja na athibitishe kazi yake mwenyewe.” (Wagalatia 6:4) Hatuwezi kudhibiti maneno au matendo ya mtu mwingine, lakini tunaweza kuamua jinsi tutakavyotenda. Kuweka kinyongo si suluhisho.

 UNACHOWEZA KUFANYA

Chukua hatua. Ni rahisi kumlaumu mwenzi wako. Lakini kumbuka, wewe ndiye unayeamua kuwa na kinyongo. Ndivyo ilivyo pia na kusamehe. Unaweza kufuata himizo hili la Biblia: “Jua lisitue [u]kiwa katika hali ya kuchokozeka.” (Waefeso 4:26) Ukiwa tayari kusamehe utafanikiwa kutatua matatizo yako ya ndoa kwa njia ya utulivu.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:13.
Jichunguze kwa unyoofu. Biblia inasema kuna watu wenye “hasira” na wenye “mwelekeo wa ghadhabu.” (Methali 29:22) Je, wewe uko hivyo? Jiulize hivi: ‘Je, nina uchungu moyoni? Je, mimi hukasirika haraka? Je, mimi hukasirishwa na mambo madogo-madogo?’ Biblia inasema kwamba “anayeendelea kuongea juu ya jambo anawatenganisha watu wanaofahamiana.” (Methali 17:9; Mhubiri 7:9) Hilo linaweza pia kutokea katika ndoa. Basi, kama una mwelekeo wa kuweka kinyongo, jiulize, ‘Je, ninaweza kuwa mwenye subira zaidi kumwelekea mwenzi wangu?’—Kanuni ya Biblia: 1 Petro 4:8.
Amua jambo muhimu zaidi. Biblia inasema kuna “wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema.” (Mhubiri 3:7) Si lazima uzungumzie kila kosa; wakati mwingine unaweza ‘kusema moyoni mwako, ukiwa kitandani mwako, na kunyamaza.’ (Zaburi 4:4) Unapohitaji kuzungumzia tatizo fulani, subiri mpaka hasira yako ishuke. Mke anayeitwa Beatriz anasema: “Ninapokasirika, mimi hujitahidi kutulia kwanza. Hatimaye, mimi huona kwamba halikuwa tatizo kubwa, na inakuwa rahisi kwangu kuzungumza kwa heshima.”—Kanuni ya Biblia: Methali 19:11.
Elewa maana ya “kusamehe.” Katika Biblia, wakati mwingine neno “kusamehe” hutafsiriwa kutokana na neno la awali linalomaanisha kuachilia kitu fulani. Kwa hiyo, kusamehe hakumaanishi kupuuza kosa kana kwamba halikutokea; kunamaanisha kuachilia kosa. Kwa sababu unatambua kwamba kuweka kinyongo kunaweza kukudhuru kiafya na kuvuruga ndoa yako hata kuliko kosa lenyewe.
Posted on : [0] comments Label: ,

UNAWEZAJE KUTHIBITI MATUMIZI YA FAMILIA

by : Unknown

AMKENI! JUNI 2014

Familia changa wakiwa katika ununuzi


KIKWAZO

Unapotazama orodha yako ya mapato na matumizi unatambua kwamba pesa zinakuponyoka kama mchanga unavyopita katikati ya vidole. Muda mrefu haujapita tangu ulipofunga ndoa, na unashindwa kudhibiti matumizi. Je, utamlaumu mwenzi wako? Usikimbilie kufanya hivyo! Shirikiana naye kuchunguza mambo ambayo huenda yamewaingiza nyote wawili katika hali hiyo. *

KISABABISHI NI NINI?

Mabadiliko. Kama ulikuwa ukiishi nyumbani kabla ya kuolewa, huenda hukuzoea kulipa gharama za nyumbani na kuchangia malipo. Inawezekana pia kwamba wewe na mwenzi wako mna maoni yanayotofautiana kuhusu pesa. Kwa mfano, huenda mmoja wenu anapenda sana kutumia pesa na yule mwingine anapenda kuweka akiba. Inachukua muda kabla wenzi wa ndoa kufanya marekebisho na kukubaliana jinsi watakavyopangia matumizi ya pesa.
Magugu yanaota na kuwazunguka wenzi wa ndoa kwenye miguu yao
Kama magugu kwenye bustani, madeni yanayopuuzwa yatazidi kuongezeka
Kuahirisha mambo. Jim, ambaye sasa ni mwanabiashara mwenye mafanikio, anakiri kwamba mara tu baada ya kufunga ndoa, alisumbuka sana kwa kushindwa kudhibiti matumizi. Anasema: “Kwa vile nilichelewa kulipa gharama za nyumbani, mimi na mke wangu tulitumia pesa nyingi kulipia gharama zilizochelewa. Tuliishiwa na pesa!”
Mtego “usioonekana wa pesa.” Ni rahisi kutumia pesa kupita kiasi kama huoni zikitoka kwenye kibeti chako. Huenda ikawa hivyo ikiwa unatumia kadi ya benki kulipia gharama mbalimbali, au unanunua bidhaa kupitia Intaneti. Mtego wa kupata mkopo haraka unaweza pia kuwanasa wenzi wapya wa ndoa.
Vyovyote vile, matumizi ya pesa yanaweza kusababisha matatizo makubwa katika ndoa yako. “Watu wengi waliofunga ndoa husema kwamba pesa ndilo tatizo kubwa, bila kuzingatia kiasi walicho nacho,” kinasema kitabu Fighting for Your Marriage. “Pesa ndicho kisababishi kikuu cha mizozano.”

 UNACHOWEZA KUFANYA

Amueni kushirikiana. Badala ya kulaumiana, shirikianeni kudhibiti matumizi yenu ya pesa. Anzeni kwa kukubaliana kwamba hamtaruhusu matumizi ya pesa yawatenganishe.—Kanuni ya Biblia: Waefeso 4:32.
Pangeni bajeti. Andikeni gharama zenu zote kwa mwezi mmoja, kutia ndani gharama ndogondogo. Hilo litawasaidia kujua matumizi yenu ya pesa na kutambua matumizi yasiyofaa. “Lazima uache kumwaga pesa,” anasema Jim aliyetajwa mapema. “Yaani ujizuie kabisa.”
Andika orodha ya malipo muhimu, kutia ndani chakula, nguo, kodi au malipo ya nyumba, gharama za gari, na mambo kama hayo. Andika kiwango kinachohitajika kwenye kila sehemu, ili kuonyesha pesa mtakazotumia katika kipindi fulani, labda kwa mwezi.—Kanuni ya Biblia: Luka 14:28.
“Mkopaji ni mtumishi wa mtu anayemkopesha.”Methali 22:7
Tenga pesa kila mwezi kwa ajili ya kila matumizi (chakula, kodi, mafuta ya gari, na kadhalika). Watu fulani hufanya hivyo kwa kuweka pesa kwenye bahasha, kila bahasha kwa matumizi hususa. * Pesa zikiisha kwenye bahasha moja, wataacha kununua vitu vilivyotengewa bahasha hiyo au kuchukua pesa kutoka kwenye bahasha nyingine.
Fikiria upya maoni yako kuhusu vitu vya kimwili. Furaha haitegemei kuwa na vifaa vya kisasa. Yesu alisema: “Hata wakati mtu ana vitu vingi uzima wake hautokani na vitu alivyo navyo.” (Luka 12:15) Kwa kawaida matumizi yako ya pesa yanaonyesha kama unaamini maneno hayo.—Kanuni ya Biblia: 1 Timotheo 6:8.
Fanya marekebisho. “Ingawa huenda mambo kama kuwa na televisheni ya kisasa na kula hotelini yakaonekana yasiyogharimu mno, yanaweza kukuvuruga kifedha,” anasema Aaron, ambaye amekuwa katika ndoa kwa miaka miwili. “Tulilazimika kujinyima mambo fulani ili tuishi kulingana na mapato yetu.”

Maelezo ya Chini

^ fu. 4 Ingawa makala hii inawalenga wale ambao wamefunga ndoa hivi karibuni, kanuni zinazotajwa zinawahusu wote waliofunga ndoa.
^ fu. 14 Kama unalipia vitu kwa kutumia kadi ya benki, weka orodha ya matumizi katika kila bahasha.
Posted on : Thursday, March 26, 2015 [0] comments Label:

UNAWEZAJE KUWAWALEA WATOTO KATIKA ULIMWENGU WENYE UBINAFSI

by : Unknown

Kulea Watoto Wenye Kujali Katika Ulimwengu Wenye Ubinafsi


KILA siku watu hupata fursa nyingi za kuwatendea wengine kwa fadhili. Hata hivyo, inaonekana kwamba watu wengi hujifikiria tu. Unaweza kuona jambo hilo kila mahali—jinsi watu wanavyowapunja wengine bila aibu, jinsi wanavyoendesha magari bila kujali, jinsi wanavyotumia lugha chafu na wanavyolipuka kwa hasira.
Mtazamo wa “mimi kwanza” pia unaonekana katika familia nyingi. Kwa mfano, wenzi fulani hutalikiana kwa sababu tu mwenzi mmoja anahisi anastahili kuwa na mtu bora kuliko yule aliye naye sasa. Bila kujua, wazazi wengine pia wanaweza kukuza mtazamo wa ubinafsi katika watoto wao. Jinsi gani? Kwa kumpa mtoto chochote anachotaka, na kusita kumpa nidhamu yoyote.
Tofauti na hilo, wazazi wengi wanawazoeza watoto wao kutanguliza masilahi ya wengine, na wanapata faida kubwa. Watoto wanaowajali wengine wanaweza kuanzisha na kufurahia urafiki wenye kudumu. Pia wanaweza kuwa na uradhi. Kwa nini? Kwa sababu kama Biblia inavyosema, “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.
Ikiwa wewe ni mzazi, unawezaje kuwasaidia watoto wako wapate faida za kuwa wenye fadhili na waepuke kuathiriwa na mtazamo wa kujifikiria ambao umeenea? Chunguza mambo matatu yanayoweza kumfanya mtoto wako awe na mtazamo wa “mimi kwanza,” na jinsi ambavyo unaweza kuyaepuka.

 1 Kumsifu Mtoto Kupita Kiasi

Tatizo. Watafiti wameona mwelekeo usiofaa: Vijana wengi wanapoanza kufanya kazi wanakuwa na mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu—mtazamo huo unawafanya wadai mafanikio hata ikiwa hawajafanya chochote kustahili mafanikio hayo. Baadhi yao hudhani kwamba watapandishwa cheo haraka, hata kabla ya kuwa stadi katika kazi yao. Wengine wanajiona kuwa bora na kwamba wanastahili kutendewa hivyo—wasipotendewa hivyo, wanashuka moyo.
Kisababishi ni nini? Nyakati nyingine huenda mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu ukatokana na malezi ya mtu. Kwa mfano, wazazi fulani wameathiriwa sana na wazo ambalo limeendelezwa katika miaka ya karibuni kwamba kujiheshimu ndilo jambo muhimu zaidi na linapaswa kuzingatiwa. Ilisemekana kwamba wazo hilo linafaa kwa kuwa ikiwa mtoto anafaidika anaposifiwa kidogo, basi akisifiwa sana atafaidika zaidi. Kwa upande mwingine, ilisemekana kwamba kumwonyesha mtoto kwamba hufurahishwi na mambo anayofanya kutamvunja moyo. Na mzazi aliyefanya hivyo alionwa kuwa mzazi asiyefaa kwani ulimwengu ulikuwa na lengo la kuwafanya watu wajiheshimu. Wazazi waliambiwa kwamba hawapaswi kumfanya mtoto ahisi kuwa amekosea.
Kwa sababu hiyo, wazazi wengi walianza kuwasifu sana watoto wao hata wakati ambapo hawakufanya jambo lolote linalostahili sifa. Mtoto alipotimiza jambo lolote, hata liwe dogo kiasi gani, alisifiwa; alipofanya makosa, hata yawe makubwa kiasi gani, yalipuuzwa. Wazazi waliamini kwamba siri ya kumfanya mtoto ajiheshimu ni kupuuza makosa na kusifu jambo lingine lolote. Kuwafanya watoto wajihisi vizuri kukawa jambo muhimu zaidi kuliko kuwafundisha kujitahidi kutimiza mambo ambayo yatawafanya wajihisi vizuri.
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba mtu anapaswa kusifiwa anapostahili. (Mathayo 25:19-21) Lakini kuwasifu watoto ili tu wajihisi vizuri kunaweza kuwafanya wawe na maoni yasiyofaa kujihusu. Biblia inasema hivi kwa kufaa: “Yeyote akifikiri kuwa yeye ni kitu wakati yeye si kitu, anaidanganya akili yake mwenyewe.” (Wagalatia 6:3) Kuna sababu nzuri kwa nini Biblia inawaambia wazazi: “Usimnyime mvulana nidhamu. Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa.” *Methali 23:13.
Mambo unayoweza kufanya. Fanya iwe lengo lako kumrekebisha mtoto inapohitajiwa na kumsifu anapostahili kikweli. Usiwasifu watoto kwa sababu tu unataka kuwafanya wajihisi vizuri. Huenda hawatafaidika. Kitabu Generation Me kinasema: “Mtu hujiheshimu kikweli kwa sababu ya kuboresha vipawa vyake na kujifunza mambo, hajiheshimu kwa sababu tu ya kusifiwa bila sababu.”
“Msijifikirie kuwa watu wa juu kuliko mlivyo. Badala yake, muwe na kiasi.”—Warumi 12:3, Neno—Agano Jipya

 2 Kumlinda Kupita Kiasi

Tatizo. Imeonekana kwamba vijana wengi huwa hawajajitayarisha kukabiliana na matatizo wanapoanza kufanya kazi. Wengine huvunjika moyo sana wanapochambuliwa kidogo tu. Wengine hawakubali kufanya kazi yoyote isipokuwa ile inayowapendeza. Kwa mfano, katika kitabu Escaping the Endless Adolescence, Dakt. Joseph Allen anasimulia kuhusu kijana mmoja ambaye alimwambia hivi alipokuwa akimhoji kwa ajili ya kazi fulani: “Ninaona kwamba sehemu fulani za kazi hii zinaweza kunichosha, nami sitaki kuchoka.” Dakt. Allen anaandika hivi: “Inaonekana hakuelewa kwamba kazi zote huwa na mambo fulani yanayochosha. Mtu anawezaje kuwa na umri wa miaka 23 na asijue jambo hilo?”
Kisababishi ni nini? Katika miaka ya hivi karibuni, wazazi wengi wameamua kuwalinda watoto wao kutokana na matatizo ya aina yoyote. Kwa sababu hiyo, binti yao anapopata alama za chini katika mtihani, wazazi huingilia kati na kumlazimisha mwalimu ampe alama za juu. Au, mwana wao anapoharibu kitu fulani anapocheza, wazazi huingilia na kumlipia. Au mwana wao anapozozana na rafiki yake, wazazi humlaumu rafiki yake.
Ingawa ni jambo la kawaida kutaka kuwalinda watoto wako, unapowalinda kupita kiasi unaweza kuwafunza jambo lisilofaa—kwamba hawahitaji kuwajibika kwa matendo yao. “Badala ya kujifunza kwamba wanaweza kukabiliana na uchungu na mambo yanayokatisha tamaa, na kujifunza jambo fulani kutokana nayo,” kinasema kitabu Positive Discipline for Teenagers, “watoto [hao] huwa watu wazima ambao ni wenye ubinafsi sana, wakiwa na maoni ya kwamba kila mtu, kutia ndani wazazi wao, wanapaswa kuwatimizia mahitaji yao.”

Biblia inasema nini? Matatizo ni sehemu ya maisha. Kwa kweli Biblia inasema: “Mambo mabaya huwapata watu wote!” (Mhubiri 9:11, Easy-to-Read Version) Hilo linatia ndani watu wazuri. Kwa mfano, Paulo, mtume Mkristo alivumilia matatizo ya aina mbalimbali alipokuwa akihubiri. Hata hivyo, kukabiliana na matatizo hayo kulimletea faida! Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwa mwenye kujitosheleza katika hali zozote nilizo nazo. . . . Nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kupatwa na uhitaji.”—Wafilipi 4:11, 12.
Mambo unayoweza kufanya. Ukizingatia ukomavu wa watoto wako, jitahidi kufuata kanuni hii ya Biblia: “Kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) Mwana wako akiharibu kitu fulani anapocheza, ingefaa umwache alipie kitu hicho. Binti yako akipata alama za chini katika mtihani, huenda hilo litaamsha fikira zake na atajitayarisha vizuri wakati ujao. Mwana wako akizozana na rafiki yake, mfariji—lakini kwa wakati unaofaa msaidie ajichunguze kwa kujiuliza, ‘Ninapotafakari hali iliyotokea, je, nilichangia kwa njia yoyote mzozano huo?’ Watoto ambao hujifunza kutatua matatizo yao huwa imara na wanajiamini zaidi—sifa ambazo hawatajifunza ikiwa mtu fulani atawatatulia matatizo yao kila wakati.
“Kila mmoja na athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi.”—Wagalatia 6:4

 3 Kuwanunulia Vitu Kupita Kiasi

Tatizo. Katika utafiti uliofanyiwa vijana, asilimia 81 walisema kwamba lengo muhimu sana katika kizazi chao ni ‘kuwa tajiri’—na waliona jambo hilo kuwa muhimu zaidi kuliko kuwasaidia wengine. Lakini kufuatilia utajiri hakumfanyi mtu aridhike. Kwa kweli, utafiti umeonyesha kwamba watu wanaokazia fikira mali hawana furaha sana na wameshuka moyo zaidi. Pia wana uwezekano mkubwa wa kuwa na matatizo ya kimwili na ya kiakili.
Kisababishi ni nini? Katika visa fulani, watoto wanalelewa katika familia zinazofuatilia mali. Kitabu The Narcissism Epidemic kinasema: “Wazazi wanataka kuwafurahisha watoto wao, nao watoto wanataka vitu vya kimwili. Kwa hiyo, wazazi huwanunulia vitu hivyo. Nao watoto wanakuwa na furaha lakini kwa muda mfupi tu. Kisha wanataka vitu zaidi.”
Bila shaka, kupitia matangazo ya kibiashara, wafanyabiashara wametumia vibaya mwelekeo huo wa kupenda kununua vitu. Wameendeleza wazo la kwamba ‘Lazima upate kilicho bora’ na ‘Unastahili kilicho bora.’ Vijana wengi wamepumbazwa na ujumbe huo na sasa wana madeni kwa sababu wameshindwa kulipia vitu hivyo ambavyo eti ‘lazima wavipate.’
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba pesa ni muhimu. (Mhubiri 7:12) Wakati huohuo, inaonya kwamba “Kupenda pesa ni chanzo cha mambo mabaya ya namna zote.” Inaongezea hivi: “Kwa kujitahidi kufikia upendo huo wengine . . . wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.” (1 Timotheo 6:10) Biblia inatutia moyo tusifuatilie utajiri bali turidhike na mahitaji muhimu ya maisha.—1 Timotheo 6:7, 8.
“Wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka katika jaribu na mtego na tamaa nyingi za kijinga na zenye kudhuru.”—1 Timotheo 6:9
Mambo unayoweza kufanya. Ukiwa mzazi, chunguza mtazamo wako kuelekea pesa na vitu ambavyo unaweza kununua ukiwa na pesa. Tanguliza mambo yanayofaa na uwasaidie watoto wako kufanya hivyo pia. Kitabu Narcissism Epidemic kilichonukuliwa kwenye makala hii kinapendekeza hivi: “Wazazi na watoto wanaweza kuzungumzia mambo kama vile ‘Ni wakati gani ni jambo la hekima kununua vitu vilivyopunguzwa bei? Ni wakati gani si jambo la hekima kufanya hivyo?’ ‘Riba ni nini?’ ‘Ni lini ulinunua kitu fulani kwa sababu tu mtu fulani alikuambia ukinunue?’”
Uwe mwangalifu usitumie vitu vya kimwili kufunika matatizo ya familia ambayo yanapaswa kushughulikiwa. Kitabu The Price of Privilege kinasema hivi: “Kutumia vitu vya kimwili kutuliza matatizo hakutayasuluhisha: matatizo yanahitaji kusuluhishwa kwa kutumia akili, ufahamu, na hisia-mwenzi, si kwa kununua viatu na vibeti.”

Kulea Watoto Wenye Kujali Katika Ulimwengu Wenye Ubinafsi

KILA siku watu hupata fursa nyingi za kuwatendea wengine kwa fadhili. Hata hivyo, inaonekana kwamba watu wengi hujifikiria tu. Unaweza kuona jambo hilo kila mahali—jinsi watu wanavyowapunja wengine bila aibu, jinsi wanavyoendesha magari bila kujali, jinsi wanavyotumia lugha chafu na wanavyolipuka kwa hasira.
Mtazamo wa “mimi kwanza” pia unaonekana katika familia nyingi. Kwa mfano, wenzi fulani hutalikiana kwa sababu tu mwenzi mmoja anahisi anastahili kuwa na mtu bora kuliko yule aliye naye sasa. Bila kujua, wazazi wengine pia wanaweza kukuza mtazamo wa ubinafsi katika watoto wao. Jinsi gani? Kwa kumpa mtoto chochote anachotaka, na kusita kumpa nidhamu yoyote.
Tofauti na hilo, wazazi wengi wanawazoeza watoto wao kutanguliza masilahi ya wengine, na wanapata faida kubwa. Watoto wanaowajali wengine wanaweza kuanzisha na kufurahia urafiki wenye kudumu. Pia wanaweza kuwa na uradhi. Kwa nini? Kwa sababu kama Biblia inavyosema, “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.
Ikiwa wewe ni mzazi, unawezaje kuwasaidia watoto wako wapate faida za kuwa wenye fadhili na waepuke kuathiriwa na mtazamo wa kujifikiria ambao umeenea? Chunguza mambo matatu yanayoweza kumfanya mtoto wako awe na mtazamo wa “mimi kwanza,” na jinsi ambavyo unaweza kuyaepuka.

 1 Kumsifu Mtoto Kupita Kiasi

Tatizo. Watafiti wameona mwelekeo usiofaa: Vijana wengi wanapoanza kufanya kazi wanakuwa na mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu—mtazamo huo unawafanya wadai mafanikio hata ikiwa hawajafanya chochote kustahili mafanikio hayo. Baadhi yao hudhani kwamba watapandishwa cheo haraka, hata kabla ya kuwa stadi katika kazi yao. Wengine wanajiona kuwa bora na kwamba wanastahili kutendewa hivyo—wasipotendewa hivyo, wanashuka moyo.
Kisababishi ni nini? Nyakati nyingine huenda mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu ukatokana na malezi ya mtu. Kwa mfano, wazazi fulani wameathiriwa sana na wazo ambalo limeendelezwa katika miaka ya karibuni kwamba kujiheshimu ndilo jambo muhimu zaidi na linapaswa kuzingatiwa. Ilisemekana kwamba wazo hilo linafaa kwa kuwa ikiwa mtoto anafaidika anaposifiwa kidogo, basi akisifiwa sana atafaidika zaidi. Kwa upande mwingine, ilisemekana kwamba kumwonyesha mtoto kwamba hufurahishwi na mambo anayofanya kutamvunja moyo. Na mzazi aliyefanya hivyo alionwa kuwa mzazi asiyefaa kwani ulimwengu ulikuwa na lengo la kuwafanya watu wajiheshimu. Wazazi waliambiwa kwamba hawapaswi kumfanya mtoto ahisi kuwa amekosea.
Kwa sababu hiyo, wazazi wengi walianza kuwasifu sana watoto wao hata wakati ambapo hawakufanya jambo lolote linalostahili sifa. Mtoto alipotimiza jambo lolote, hata liwe dogo kiasi gani, alisifiwa; alipofanya makosa, hata yawe makubwa kiasi gani, yalipuuzwa. Wazazi waliamini kwamba siri ya kumfanya mtoto ajiheshimu ni kupuuza makosa na kusifu jambo lingine lolote. Kuwafanya watoto wajihisi vizuri kukawa jambo muhimu zaidi kuliko kuwafundisha kujitahidi kutimiza mambo ambayo yatawafanya wajihisi vizuri.
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba mtu anapaswa kusifiwa anapostahili. (Mathayo 25:19-21) Lakini kuwasifu watoto ili tu wajihisi vizuri kunaweza kuwafanya wawe na maoni yasiyofaa kujihusu. Biblia inasema hivi kwa kufaa: “Yeyote akifikiri kuwa yeye ni kitu wakati yeye si kitu, anaidanganya akili yake mwenyewe.” (Wagalatia 6:3) Kuna sababu nzuri kwa nini Biblia inawaambia wazazi: “Usimnyime mvulana nidhamu. Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa.” *Methali 23:13.
Mambo unayoweza kufanya. Fanya iwe lengo lako kumrekebisha mtoto inapohitajiwa na kumsifu anapostahili kikweli. Usiwasifu watoto kwa sababu tu unataka kuwafanya wajihisi vizuri. Huenda hawatafaidika. Kitabu Generation Me kinasema: “Mtu hujiheshimu kikweli kwa sababu ya kuboresha vipawa vyake na kujifunza mambo, hajiheshimu kwa sababu tu ya kusifiwa bila sababu.”
“Msijifikirie kuwa watu wa juu kuliko mlivyo. Badala yake, muwe na kiasi.”—Warumi 12:3, Neno—Agano Jipya

 2 Kumlinda Kupita Kiasi

Tatizo. Imeonekana kwamba vijana wengi huwa hawajajitayarisha kukabiliana na matatizo wanapoanza kufanya kazi. Wengine huvunjika moyo sana wanapochambuliwa kidogo tu. Wengine hawakubali kufanya kazi yoyote isipokuwa ile inayowapendeza. Kwa mfano, katika kitabu Escaping the Endless Adolescence, Dakt. Joseph Allen anasimulia kuhusu kijana mmoja ambaye alimwambia hivi alipokuwa akimhoji kwa ajili ya kazi fulani: “Ninaona kwamba sehemu fulani za kazi hii zinaweza kunichosha, nami sitaki kuchoka.” Dakt. Allen anaandika hivi: “Inaonekana hakuelewa kwamba kazi zote huwa na mambo fulani yanayochosha. Mtu anawezaje kuwa na umri wa miaka 23 na asijue jambo hilo?”
Kisababishi ni nini? Katika miaka ya hivi karibuni, wazazi wengi wameamua kuwalinda watoto wao kutokana na matatizo ya aina yoyote. Kwa sababu hiyo, binti yao anapopata alama za chini katika mtihani, wazazi huingilia kati na kumlazimisha mwalimu ampe alama za juu. Au, mwana wao anapoharibu kitu fulani anapocheza, wazazi huingilia na kumlipia. Au mwana wao anapozozana na rafiki yake, wazazi humlaumu rafiki yake.
Ingawa ni jambo la kawaida kutaka kuwalinda watoto wako, unapowalinda kupita kiasi unaweza kuwafunza jambo lisilofaa—kwamba hawahitaji kuwajibika kwa matendo yao. “Badala ya kujifunza kwamba wanaweza kukabiliana na uchungu na mambo yanayokatisha tamaa, na kujifunza jambo fulani kutokana nayo,” kinasema kitabu Positive Discipline for Teenagers, “watoto [hao] huwa watu wazima ambao ni wenye ubinafsi sana, wakiwa na maoni ya kwamba kila mtu, kutia ndani wazazi wao, wanapaswa kuwatimizia mahitaji yao.”
Biblia inasema nini? Matatizo ni sehemu ya maisha. Kwa kweli Biblia inasema: “Mambo mabaya huwapata watu wote!” (Mhubiri 9:11, Easy-to-Read Version) Hilo linatia ndani watu wazuri. Kwa mfano, Paulo, mtume Mkristo alivumilia matatizo ya aina mbalimbali alipokuwa akihubiri. Hata hivyo, kukabiliana na matatizo hayo kulimletea faida! Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwa mwenye kujitosheleza katika hali zozote nilizo nazo. . . . Nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kupatwa na uhitaji.”—Wafilipi 4:11, 12.
Mambo unayoweza kufanya. Ukizingatia ukomavu wa watoto wako, jitahidi kufuata kanuni hii ya Biblia: “Kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) Mwana wako akiharibu kitu fulani anapocheza, ingefaa umwache alipie kitu hicho. Binti yako akipata alama za chini katika mtihani, huenda hilo litaamsha fikira zake na atajitayarisha vizuri wakati ujao. Mwana wako akizozana na rafiki yake, mfariji—lakini kwa wakati unaofaa msaidie ajichunguze kwa kujiuliza, ‘Ninapotafakari hali iliyotokea, je, nilichangia kwa njia yoyote mzozano huo?’ Watoto ambao hujifunza kutatua matatizo yao huwa imara na wanajiamini zaidi—sifa ambazo hawatajifunza ikiwa mtu fulani atawatatulia matatizo yao kila wakati.
“Kila mmoja na athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi.”—Wagalatia 6:4

 3 Kuwanunulia Vitu Kupita Kiasi

Tatizo. Katika utafiti uliofanyiwa vijana, asilimia 81 walisema kwamba lengo muhimu sana katika kizazi chao ni ‘kuwa tajiri’—na waliona jambo hilo kuwa muhimu zaidi kuliko kuwasaidia wengine. Lakini kufuatilia utajiri hakumfanyi mtu aridhike. Kwa kweli, utafiti umeonyesha kwamba watu wanaokazia fikira mali hawana furaha sana na wameshuka moyo zaidi. Pia wana uwezekano mkubwa wa kuwa na matatizo ya kimwili na ya kiakili.
Kisababishi ni nini? Katika visa fulani, watoto wanalelewa katika familia zinazofuatilia mali. Kitabu The Narcissism Epidemic kinasema: “Wazazi wanataka kuwafurahisha watoto wao, nao watoto wanataka vitu vya kimwili. Kwa hiyo, wazazi huwanunulia vitu hivyo. Nao watoto wanakuwa na furaha lakini kwa muda mfupi tu. Kisha wanataka vitu zaidi.”
Bila shaka, kupitia matangazo ya kibiashara, wafanyabiashara wametumia vibaya mwelekeo huo wa kupenda kununua vitu. Wameendeleza wazo la kwamba ‘Lazima upate kilicho bora’ na ‘Unastahili kilicho bora.’ Vijana wengi wamepumbazwa na ujumbe huo na sasa wana madeni kwa sababu wameshindwa kulipia vitu hivyo ambavyo eti ‘lazima wavipate.’
Biblia inasema nini? Biblia inakubali kwamba pesa ni muhimu. (Mhubiri 7:12) Wakati huohuo, inaonya kwamba “Kupenda pesa ni chanzo cha mambo mabaya ya namna zote.” Inaongezea hivi: “Kwa kujitahidi kufikia upendo huo wengine . . . wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.” (1 Timotheo 6:10) Biblia inatutia moyo tusifuatilie utajiri bali turidhike na mahitaji muhimu ya maisha.—1 Timotheo 6:7, 8.
“Wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka katika jaribu na mtego na tamaa nyingi za kijinga na zenye kudhuru.”—1 Timotheo 6:9
Mambo unayoweza kufanya. Ukiwa mzazi, chunguza mtazamo wako kuelekea pesa na vitu ambavyo unaweza kununua ukiwa na pesa. Tanguliza mambo yanayofaa na uwasaidie watoto wako kufanya hivyo pia. Kitabu Narcissism Epidemic kilichonukuliwa kwenye makala hii kinapendekeza hivi: “Wazazi na watoto wanaweza kuzungumzia mambo kama vile ‘Ni wakati gani ni jambo la hekima kununua vitu vilivyopunguzwa bei? Ni wakati gani si jambo la hekima kufanya hivyo?’ ‘Riba ni nini?’ ‘Ni lini ulinunua kitu fulani kwa sababu tu mtu fulani alikuambia ukinunue?’”
Uwe mwangalifu usitumie vitu vya kimwili kufunika matatizo ya familia ambayo yanapaswa kushughulikiwa. Kitabu The Price of Privilege kinasema hivi: “Kutumia vitu vya kimwili kutuliza matatizo hakutayasuluhisha: matatizo yanahitaji kusuluhishwa kwa kutumia akili, ufahamu, na hisia-mwenzi, si kwa kununua viatu na vibeti.”
(Source: JW)
Posted on : [0] comments Label:

MTOTO ANAWEZAJE KUBORESHA NDOA

by : Unknown
“Wana ni urithi kutoka kwa Yehova.” Zaburi 127:3
Mtoto anapozaliwa, huenda kikawa kipindi cha kusisimua na chenye mkazo kwa mume na mke. Mkiwa wazazi wapya, huenda mkatumia muda mwingi kumtunza na kumlea mtoto wenu. Huenda kukosa usingizi na mabadiliko ya kihisia yakaleta mkazo kwenye ndoa yenu. Nyote wawili mnapaswa kufanya marekebisho ili mfanikiwe kumlea mtoto na pia kudumisha ndoa yenu. Ushauri wa Biblia unawezaje kuwasaidia mfanikiwe?

 1 ELEWA JINSI MTOTO ANAVYOBADILI MAISHA YENU

BIBLIA INASEMA HIVI: “Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili.” Pia, upendo “hautafuti faida zake wenyewe, hauchokozeki.” (1 Wakorintho 13:4, 5) Ukiwa mama mpya, utatumia muda mwingi kumtunza mtoto wako. Hata hivyo, huenda mume wako akaanza kuhisi amepuuzwa, kwa hiyo usisahau kwamba yeye pia anahitaji kukaziwa fikira. Kwa subira na fadhili, unaweza kumsaidia ahisi anathaminiwa na anahusika katika kumlea mtoto wenu.
Baba akimlisha mtoto chakula, na akimtunza wakati wa usiku
“Enyi waume, endeleeni kukaa nao . . . kulingana na ujuzi.” (1 Petro 3:7) Elewa kwamba mke wako atatumia muda mwingi kumtunza mtoto wenu. Kwa sababu ana jukumu jipya huenda akawa na mkazo, uchovu na hata kushuka moyo. Nyakati nyingine, huenda akakukasirikia, lakini uwe mtulivu, kwa sababu mtu “asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu.” (Methali 16:32) Uwe mwenye utambuzi na umpe msaada anaohitaji. Methali 14:29.
UNACHOWEZA KUFANYA:
  • Baba: Msaidie mke wako kumtunza mtoto, hata kama ni usiku. Punguza muda unaotumia kufanya mambo mengine ili upate muda zaidi wa kuwa na mkeo pamoja na mtoto
  • Mama: Mume wako anapojitolea kumtunza mtoto, kubali msaada wake. Ikiwa hafanyi vizuri, usimkosoe, badala yake kwa fadhili mwelekeze jinsi anavyopaswa kufanya

 2 IMARISHENI UHUSIANO WENU

BIBLIA INASEMA HIVI: “Watakuwa mwili mmoja.” (Mwanzo 2:24) Ingawa mmepata mtu mpya kwenye familia yenu, kumbuka kwamba wewe na mwenzi wako bado ni “mwili mmoja.” Jitahidini kuimarisha uhusiano wenu.
Mke, mshukuru mume wako kwa msaada na utegemezo wake. Maneno yako ya shukrani yanaweza ‘kuponya.’ (Methali 12:18) Mume, mwambie mke wako jinsi unavyompenda na kumthamini. Mpongeze mkeo kwa jinsi anavyoitunza familia.Methali 31:10, 28.
Mume na mke wakiwa pamoja wakati mtoto wao amelala
“Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali ile ya yule mtu mwingine.” (1 Wakorintho 10:24) Sikuzote jitahidi kumfanyia mwenzi wako mambo mema. Uwe na muda wa kuzungumza, kumpongeza, na kumsikiliza mwenzi wako. Msinyimane uhusiano wa kingono. Zingatia mahitaji ya mwenzi wako. Biblia inasema hivi: “Msiwe mkinyimana haki hiyo, ila kwa makubaliano.” (1 Wakorintho 7:3-5) Zungumzieni jambo hilo kwa unyoofu nyinyi wenyewe. Mkionyesha subira na utambuzi mtaimarisha ndoa yenu.
UNACHOWEZA KUFANYA:
  • Msisahau kupanga wakati wa kuwa pamoja peke yenu
  • Usisahau kufanya mambo yatakayomwonyesha mwenzi wako kwamba unampenda, kama vile kumtumia ujumbe au kumnunulia zawadi

 3 KUMZOEZA MTOTO WENU

Mama akimsomea  mtoto wake kitabu
BIBLIA INASEMA HIVI: “Tangu utoto mchanga umeyajua maandishi matakatifu, ambayo yanaweza kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu.” (2  Timotheo 3:15) Pangeni mapema jinsi mtakavyomfundisha mtoto wenu. Mtoto ana uwezo mkubwa wa kujifunza hata kabla hajazaliwa. Anapokuwa tumboni, mtoto anaweza kutambua sauti na hisia zako. Msomee hata akiwa bado mchanga. Hata kama hataelewa unachosoma, hilo litamsaidia kupenda kusoma atakapokuwa mkubwa.
Mtoto wako anaweza kuelewa unapozungumza kuhusu Mungu. Mwache asikie unaposali kwa Yehova. (Kumbukumbu la Torati 11:19) Hata unapocheza na mtoto wako, zungumza kuhusu vitu ambavyo Mungu ameumba. (Zaburi 78:3, 4) Kadiri mtoto wako anavyokua atatambua jinsi unavyompenda Yehova naye pia atajifunza kumpenda.
UNACHOWEZA KUFANYA:
  • Mwombe Yehova akupe hekima ya kumfundisha mtoto wako
  • Mtajie mtoto wako tena na tena maneno na mawazo makuu ili aanze kujifunza mapema

Posted on : Tuesday, February 10, 2015 [0] comments Label:

KIJANA UNAWEZA KUKABILIANAJE NA SHERIA ZA WAZAZI WAKO?

by : Unknown


Unahitaji: Kujua jinsi ya kuwasiliana
Mawasiliano ni muhimu ili
  • kuwasaidia wengine wakuelewe au
  • kukusaidia kuelewa ni kwa nini hauruhusiwi kufanya unachotaka.
Kwa kweli, ukitaka utendewe kama mtu mzima, basi lazima ujifunze kuwasiliana kama mtu mzima. Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?
Jifunze kuzuia hisia zako. Ili kuwasiliana vizuri, lazima uwe na sifa ya kujizuia. Biblia inasema: “Mtu mjinga huiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima huituliza mpaka mwisho.”Methali 29:11.
Hilo linatufundisha nini? Epuka kulialia, kununanuna, kubamiza mlango, au kupigapiga miguu chini eti kwa sababu una hasira. Tabia kama hiyo itafanya wazazi wako wakuwekee sheria nyingine, badala ya kukupa uhuru zaidi.
Jaribu kuelewa maoni ya wazazi wako. Kwa mfano: Tuseme wazazi wako wanasita kukupa ruhusa ya kwenda kujumuika na vijana wengine. Badala ya kubishana nao, unaweza kuwauliza:
“Vipi ikiwa nitaandamana na rafiki mkomavu na mwenye kutumainika?”
Huenda bado wazazi wako wakakataa. Hata hivyo, ukielewa hangaiko lao, huenda ukapendekeza jambo ambalo labda watakubali.
Kutii sheria za wazazi wako ni kama kulipa mkopo wa benki, kadiri unavyolipa kwa wakati ndivyo unavyoaminika zaidi.
Jiendeshe kwa njia itakayofanya wazazi wako wakuamini zaidi.Wazia mtu amechukua mkopo katika benki. Akiwa na mazoea ya kulipa kwa wakati, benki itamwamini na inaweza kumpa mkopo mkubwa zaidi siku za usoni.
Ndivyo ilivyo na nyumbani. Unapaswa kuwatii wazazi wako. Ukiwatamausha wazazi wako mara kwa mara, usishangae wakikaza kamba au hata kukuzuilia kabisa.
Kwa upande mwingine, ukiwatii hata katika mambo madogo, wazazi wako watakuamini hata zaidi wakati ujao.