Latest News


More

FRANK NA HAPPY WAMEREMETA KATIKA KANISA LA ST.PETER OYSTERBAY

Posted by : Unknown on : Sunday, July 6, 2014 2 comments
Unknown
Saved under : ,




 Jana jumamosi ilikua siku ya furaha kubwa kwa bwana Frank Regis Maro pamoja na Happyness Saro baada ya kufunga ndoa katika kanisa la St.Peter Oysterbay na baadaye wakaungana na familia kwenye tafrija ya nguvu iliyofanyika katika ukumbi wa Msasani Beach Club (Makuti hall)
Pichani juu ni  maharusi wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanafamilia mara baada ya kufunga ndoa yao kanisani hapo


Maharusi wakiwa kanisani St Peter Oysterbay kwenye misa ya ndoa takatifu
Maharusi wakipata picha katika viwanja vya Hotel Golden Tulip
Maharusi wakiwa kwenye picha ya pamoja na wapambe wao kwenye bustani ya hoteli ya kitalii ya Golden Tulip
Maharusi wakiwa kwenye picha ya pozi
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ambaye pia alikua Floor Manager Bwana Tumaini Kichila akiwakaribisha wageni kwenye sherehe hiyo
Bi harusi Happyness akikabidhi keki kwa wazazi wa bwana harusi
Maharusi wakikabidhi keki kwa mwenyekiti wa kamati ya maandalizi kwa niaba ya kamati nzima
Maharusi wakilishana keki
Bwana harusi akimlisha keki msimamizi mdogo Evelyn Kichila
Mc wa sherehe hiyo Mc Makassy Junior akiwapa shampaigne maharusi
Wageni mbalimbali wakiwa kwenye sherehe hiyo
Floor Manager bwana Kichila akisaidia kukata kata ndafu
Picha ya pamoja ya wazazi na maharusi
Maharusi wakipata chakula cha usiku
Baadhi ya ndugu wa bibi harusi wakitoa mkono wa pongezi kwa maharusi
Ndugu wa bibi harusi wakitoa mkono wa pongezi kwa maharusi
Wafanyakazi wenzake wa mama wa Bwana harusi wakipeleka zawadi kwa maharusi

Ndugu wakimtunza mama wa bwana harusi


Maharusi wakiwa kwenye picha ya pamoja  na kamati ya maandalizi ya harusi mara baada ya sherehe katika ukumbi wa Msasani Beach Makuti  Hall

"Blog hii inawatakia kila la heri maharusi hawa"

2 comments: for FRANK NA HAPPY WAMEREMETA KATIKA KANISA LA ST.PETER OYSTERBAY

  1. ilipendeza sana Mungu awabariki sana.

    ReplyDelete
  2. Waaaooooh! mlipendeza saaana! Mungu awabariki maharusi

    ReplyDelete